Waziri Mwijage:Ukiwa na cherehani nne unamiliki kiwanda ...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa viwanda, biashara na uwezeshaji Charles Mwijage ameendelea kusisitiza kwamba kwa mujibu wa tafsiri ya serikali ya awamu ya tano ukiwa na cherehani nne unamiliki kiwanda.
Waziri wa viwanda, biashara na uwezeshaji Charles Mwijage katikati akiandika jambo fulani alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Amesisitiza hilo wakati alipotakiwa na kutoa tafasiri halisi ya viwanda vinavyozungumziwa.

“Na hapa tuwe makini kidogo kwa sababu kuna watu wengine wanataka kupotosha, watu wengine wanalenga kubeza na rudia kwa mara ya 26 cherehani nne kwa tafsiri yetu ya viwanda ni kiwanda kidogo,” amesema Mwijage.

Mwijage aliombwa kutoa tafsiri hiyo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam juu ya maandalizi ya maonesho ya pili ya bidhaa za viwanda  yatakayofanyika kuanzia Desemba 7  hadi 11, 2017.

Watu wamekuwa wakikosoa takwimu ambazo zimekuwa zikitolewa na waziri Mwijage kwamba tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani zaidi ya viwanda 3000 vimekwisha jengwa huku katika takwimu hizo akitaja hata mwenye cherehani nne anakiwanda.

Pia amesema lengo ni kujenga viwanda jumuishi
vitakavyotumia malighafi za ndani badala ya nje.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search