Wataalam wasema afya ya akili tatizo nchini....soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es salaam

TAFITI zinaonesha katika kila watu wanne Duniani mmoja anauwezekano  wakupata changamoto ya afya ya akili.
Daktari bingwa wa afya ya akili kutoka hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Saidi Luganda akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Hayo yameelezwa leo jijini Dar es Salaam na Daktari
bingwa wa afya ya akili kutoka hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Saidi Lunganda akizungumza na waandishi wa habari.

“Tunaposema changamoto ya afya ya akili huyu mtu si mgonjwa, maana yake  kuna jambo limemtatiza, unaweza ukawa na ugonvi na mwenzako ukapata msongo wa mawazo,” amesema Luganda.

“Msongo wa mawazo unavyokuendesha ndiyo unaweza kusababisha uwezekano wa kupata matatizo ya kiakili,” ameongeza .

Luganda ametaja baadhi ya sababu za kimaisha zinazoweza kuchangia kupata matatizo ya afya ya akili ambayo ni kufiwa, kuongezwa cheo, kuoa na kuolewa, kuachwa na kadhalika.

Akizungumzia hali ya tatizo hilo nchini, amesema ni mbaya na kueleza kuwa wamekuwa wakiwapokea  hospitalini wale tu ambao wanaonekana wazi kuathirika huku waliowengi na ambao hawaonekani wakishidwa kuripoti vituo vya afya kwa kuhofia unyanyapaa.

Amebainisha kuwa mara nyingi afya ya akili inapoathirika na mambo mengine katika maisha huathirika.

Amesema ili kukabiliana na hali hiyo jamii inatakiwa kuelimishwa na kujua athari zinazoweza  kutokea kutokana na tatizo hilo ili hatua madhubuti zichukuliwe pindi mtu anapobainika kupatia hali hiyo.

Ameeleza kwamba wengi wenye changamoto  hiyo wamekuwa wakipelekwa kwa waganga wa kienyeji na wengine kwenye maombezi bila kupata ushauri wa madaktari kwa ajili ya kujua hasa tatizo linalomsumbua mgonjwa.

“Kwa hiyo kupeleka  elimu  kwa jamii  huenda tukabadilika na kuanza kuona afya ya akili ni jambo la kawaida na kuacha kunyanyapaana,” amesema.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search