Waziri aitaka ACSAF kufikisha mawasiliano kote nchini...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Abraham Ntambara

MFUKO wa mawasiliano kwa wote (ACSAF) umetakiwa  kufikisha huduma ya mawasiliano kote nchini.

Naibu waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Atashasta Nditiye akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Naibu waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Atashasta Nditiye akizungumza na waandishi wa habari alipotembelea mfuko huo kwa lengo la kupata taarifa ya utekelezaji wa miradi ya usambazaji wa huduma ya mawasiliano.

“Mkakati wa serikali ni kuhakikisha huduma ya mawasiliano inamfikia kila mwananchi, mnatakiwa kuharakisha huduma hii katika maeneo ambayo bado hayajafikiwa, lakini jamii pia itoe ushirikiano pale wanapoona miradi ya mawasiliano inatekelezwa katika maeneo yao,” amesema Nditiye.

Naibu waziri huyo amesema kwa sasa wananchi wengi wamepata hamasa za kuhitaji mawasiliano na kusisitiza kuwa kutokana na mwamko huo juhudi za haraka zinahitajika katika kuwafikishia huduma hiyo.

Amewataka  watekelezaji wa huduma za mawasiliano kuhakikisha wanapeleka miradi hiyo maeneo yaliyokusudiwa pekee.
  
"watoa huduma hakikisheni hamfania kazi ya kupindisha miradi yaani ilipokusudiwa kupelekwa hampeleki hiyo mtakuwa hamtekelezi azma ya serikali ya kufikisha mawasiliano  kwa wote"amesema.

kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa (UCSAF)  Mhandisi Peter Ulanga amesema tangu waanze utekelezaji wa miradi ya mawasiliano kwa wote wa 2013 wameshafikia zaidi ya wananchi milioni 4.

Pia wamefikia zaidi ya vijiji 2000  na kata  444 huku  zaidi ya kata 120 zikiwa katika hatua za utekelezaji wa miradi hiyo.

"Kabla mfuko huu haujaanza ni asilimia 80 ya wananchi walikuwa wamefikiwa, lakini kwa sasa imefikia asilimia 90, inamana kwamba mfuko huu umeongeza asilimia 10 na gharama za miradi tuliyofadhili zimefikia   zaidi bilioni 85,” amesema Ulanga.

Amesema kama mfuko huu usingekuwepo zaidi ya wananchi milioni 5 wasingekuwa wamefikiwa na huduma hii.




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search