CUF Lipumba 'walia' rafu uchaguzi Kinondoni...soma habari kamili na matukio 360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

CHAMA cha Wananchi CUF upande unaomuunga mkono Mwenyekiti Profesa Ibrahim Lipumba umemteua Rajab Juma aliyekuwa kampeni meneja wa Maulid Mtulia kugombea ubunge  jimbo la Kinondoni.
Mgombea Ubunge Jimbo la Kinondoni CUF Lipumba, Rajab Juma akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuchukua fomu.

Pia mgombea huyo amelalamikia kitendo cha Mtulia anayegombea tena ubunge katika jimbo hilo kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM)  kuanza kampeni.

Malalamiko hayo ameyatoa leo akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuchukua fomu ya kugombea ubunge kwenye ofisi za halmashauri ya manispaa ya Kinondoni.

 amesema Mtulia ameanza kupita katika matawi ya CUF kuomba kuungwa mkono.

“Tumeshasainiwa fomu, isipokuwa kuna mambo ya kusikitisha sana, na sisi kama wanasiasa tumeona tuanze mapema kutoa angalizo ili muweze kutusaidia, sasa mgombea wa CCM ameanza kupita katika matawi yetu ya CUF,kwanza kipindi cha kampeni bado lakini ni makosa kwa mgombea wa chama kingine kwenda katika chama chetu,” amesema Juma.

Amesema suala hilo kama halitachukuliwa hatua litaleta athari kwani siasa siyo chuki,uadui na wamedhamiria kufanya siasa kama sehemu ya kuweza kuondoa kero ambazo zinawakabili wananchi.

Mkurugenzi wa habari na Uenezi wa CUF Lipumba, Abdul Kambaya amesema kitendo cha CCM kumteua Mtulia kuwa mgombea wao inadhihirisha kwamba kimeridhia matumizi mabaya ya fedha za umma.

“Alichokifanya Mtulia ni kutuitisha kwenyae uchaguzi mdogo usiokuwa na sababu, hakufa ni mzima, haumwi, hana tatizo la kutohudhuria bungeni, ameamua kujizulu uanachama na kupoteza nafasi ya ubunge na uchaguzi ni gharama fedha za walipakodi wa Tanzania zinakwenda kutumika kwenye uchaguzi mdogo usiokuwa na sababu,” amesema Kambaya.

Ameongeza  kuwa wanauhakika watashinda katika uchaguzi kwa kuwa wanamgombea mzuri, uwezo na  mwenye kujiamini.


Uchaguzi mdogo wa marudio katika jimbo la kinondoni unatarajiwa kufanyika Februari 17, 2018 na unafanyika baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Maulidi Mtulia kujiuzulu nafasi hiyo na kujiunga na CCM kwa madai kwamba ni kuunga juhudi za Rais John Magufuli katika kupigania rasilimali za taifa ampapo kwa sasa pia ni mgombea kupitia chama hicho.
Mgombea Ubunge Jimbo la Kindondoni CUF Rajab Juma  akikabidhiwa fomu na msimamizi msaidizi wa uchaguzi jimbo la Kinondoni Latifa Ramadhani.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search