Jalada kesi mhasibu Takukuru lapelekwa Takukuru ...soma habari kamili na matukio 360...#share
Na
Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
JALADA la kesi ya utakatishaji fedha na kumiliki mali zisizoendana na
kipato chake inayomkabili aliyekuwa mhasibu mkuu wa Takukuru, Godfrey Gugai na
wenzake watatu limepelekwa Takukuru kwa ajili ya upelelezi zaidi.
Aliyekuwa mhasibu wa Takukuru, Godfrey Gugai akitoka katika chumba cha mahakama ya hakimu mkazi Kisutu leo jijini Dar es salaam.
Wakili
wa Serikali Simon Wankyo akisaidiana na wakili Salim Msemo ameeleza leo mbele
ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, wakati shauri hilo lilipofikishwa
mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa upelelezi ikiwa haujakamilika.
Wakili
Wankyo amedai, jalada la kesi hiyo lilipelekwa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka
nchini(DPP) kwa ajili ya kusomwa na sasa limerudishwa Taasisi ya Kuzuia na
Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru) kwa ajili ya upelelezi zaidi.
Ameongeza, baada ya kukamilisha upelelezi, jalada hilo litarudishwa tena kwa DPP ili kujiridhisha kama maelekezo aliyoyatoa yamefanyiwa Kazi.
Ameongeza, baada ya kukamilisha upelelezi, jalada hilo litarudishwa tena kwa DPP ili kujiridhisha kama maelekezo aliyoyatoa yamefanyiwa Kazi.
Hata
hivyo, baada ya maelezo hayo, wakili wa Utetezi Alex Mshumbusi alidai kuwa
hategemei upelelezi kuchukua muda mrefu kwa sababu mshtakiwa Gugai alikuwa
mtumishi wa Takukuru na tayari alishashtakiwa kinidhamu na Takukuru yenyewe na
kupoteza ajira yake.
Kesi
hiyo imeahirishwa hadi Januari 31, mwaka huu itakapotajwa.
Mbali na
Gugai, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni George Makaranga, Leonard Aloys
na Yasini Katera.Washitakiwa hao wanaokabiliwa na mashitaka 43
yakiwemo 20 ya utakatishaji fedha haramu, kumiliki mali zisizoendana na kipato
na kughushi mikataba ya mauziano ya viwanja katika maeneo mbalimbali.
Katika
shitaka la kwanza ambalo ni kumiliki mali ambazo hazina maelezo ambalo
linamkabili Gugai, inadaiwa kati ya January 2005 na December 2015, jijini Dar
es Salaam, akiwa ofisa wa umma ameajiriwa na TAKUKURU anamiliki mali zenye
thamani zaidi ya Sh 3.6bilioni ambazo haziendani na kipato chake cha
sasa wala cha nyuma.
No comments:
Post a Comment