Kesi inayomkabili Mattaka kuunguruma Februari ....soma habari kamili na matukio360...#share
Na mwandishi wetu, Dar es salaam
KESI ya matumizi mabaya ya madaraka, kughushi na kusababisha hasara kupitia ukodishaji ndege inayomkabili Mkurugenzi Mtendaji wa zamani wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), David Mattaka na wenzake wawili itaendelea kuunguruma katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Februari 22,2018.
Kwa upande wa washtakiwa Mlinga na Bertha, wao wanadaiwa kuwa Machi 19,2008 katika ofisi za PPRA zilizopo wilaya ya Ilala kwa nia ya udanganyifu walighushi Muhtasari wa kikao cha siku hiyo wakionyesha mamlaka hiyo ilifanya kikao cha kujadili maombi ya ATCL juu ya kuidhinishwa kwa mkataba huo. Washtakiwa hao wapo nje kwa dhamana
KESI ya matumizi mabaya ya madaraka, kughushi na kusababisha hasara kupitia ukodishaji ndege inayomkabili Mkurugenzi Mtendaji wa zamani wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), David Mattaka na wenzake wawili itaendelea kuunguruma katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Februari 22,2018.
Kesi hiyo leo imeahirishwa kwa Hakimu Mkazi Mkuu Wilbard Mashauri hadi Februari 22,2018 ambapo mashahidi wa upande wa mashtaka wataendelea kutoa ushahidi wao.
Mbali na Mattaka washtakiwa wengine wanaokabiliwa katika kesi hiyo, inayoendeshwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Vitalis Peter mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage, ni Afisa Mtendaji Mkuu Mstaafu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA), Ramadhan Mlinga na Mwanasheria wa mamlaka hiyo, Bertha Soka.
Washtakiwa hao wanadaiwa kuwa Oktoba 9,2007 katika ofisi za ATCL zilizopo wilayani Ilala, Mattaka wakati akitekeleza majukumu yake alitumia vibaya madaraka yake kwa kutia saini kwenye mkataba wa ukodishaji wa ndege A 320-214 iliyotengenezwa kwa namba 630 baina ya Wallis Trading Inc na ATCL.
Mattaka anadaiwa kuwa alifanya hivyo bila ya kuzingatia sheria ya Manunuzi ya Umma na kutofuata taratibu za zabuni kwenye mchakato wote.
Mkurugenzi Mtendaji huyo wa zamani wa ATCL, Mattaka anadaiwa kuwa Oktoba 27,2007 alitumia vibaya madaraka yake kwa kutia saini kwenye cheti cha kuruhusu mchakato wa ukodishaji wa h ndege hiyo bila ya kufuata ushauri wa kiufundi aliokuwa amepatiwa.
Mattaka anaendelea kudaiwa kuwa kati ya Oktoba 27,2007 na Aprili 24,2008 kwenye ofisi za ATCL kutokana na kitendo chake cha kutia saini cheti hicho bila ya kuzingatia ushauri wa kiufundi alisababisha hasara ya dola za Kimarekani 772,402.08 zilizolipwa kwa kampuni ya Aeromantenimiento , S. A kama gharama za huduma ya matengenezo.
Kati ya Oktoba 27 na Novemba 29,2007 kwenye ofisi hizo za ATCL, Mattaka anadaiwa kutia kwake saini kwenye cheti hicho kulisababisha hasara ya dola za Kimarekani 35,984.82 ambazo zilizolipwa kwa kampuni ya Lantal Textiles, INC kwa ajili ya ununuaji wa mahitaji ya ndege hiyo ikiwamo Kapeti.
Iliendelea kudaiwa kuwa, kati ya Oktoba 9, 2007 na Oktoba 26, 2011, kutokana na kitendo cha Mattaka kutia saini kwenye mkataba baina ya kampuni ya Wallis Tranding Inc ya Liberia na ATCL alisababisha hasara ya dola za Kimarekani 42,459,316.12 ambazo ATCL iliilipa kampuni hiyo.
Kwa upande wa washtakiwa Mlinga na Bertha, wao wanadaiwa kuwa Machi 19,2008 katika ofisi za PPRA zilizopo wilaya ya Ilala kwa nia ya udanganyifu walighushi Muhtasari wa kikao cha siku hiyo wakionyesha mamlaka hiyo ilifanya kikao cha kujadili maombi ya ATCL juu ya kuidhinishwa kwa mkataba huo. Washtakiwa hao wapo nje kwa dhamana
No comments:
Post a Comment