Maandalizi tamasha la busara bambam....soma habari kamili na matukio360...#share
Na Abraha Ntambara, Dar es Salaam
MAANDALIZI ya tamasha la Sauti za Busara, linalotarajia kufanyika Februari 8, 2018 katika mji Mkongwe, visiwani Zanzibar yanaendelea vizuri.
MAANDALIZI ya tamasha la Sauti za Busara, linalotarajia kufanyika Februari 8, 2018 katika mji Mkongwe, visiwani Zanzibar yanaendelea vizuri.
Mkurugenzi wa Tamasha la Sauti za Busara Yusuf Mahmoud akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Tamasha hilo linatarajiwa kuanza Februari 8 hadi Februari 11,
2018 lenye kauli mbiu ya “kuunganishwa na Muziki”, Waafrika
na wageni kutoka katika kila pembe ya dunia.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo,
Mkurugenzi wa Tamasha hilo, Yusuf Mahmoud amesema tamasha linaitangaza
Zanzibar na Tanzania sehemu mbali mbali duniani kwa kuwa linavutia mapromota wa
kimataifa na kutoa fursa adhimu kwa wanamuziki wa Afrika Mashariki kuupeleka
mziki wao duniani kote.
“Ndani ya majukwaa matatu kwa siku nne, tamasha litakuwa na
maonyesho 46 yenye hadhi ya kimataifa ambayo kwa asilimia 100 yatapigwa
mbashara. Tamasha litawaweka pamoja wanamuziki wadogo na wakubwa kutoka katika
viunga vyetu na hata nje ya nchi, likibeba dhumuni moja huku tukisimama pamoja
kupitia kauli mbiu ya ‘kuunganishwa na muziki”, amesema Yusuf.
Yusuf amesema orodha ya wanamuziki imejitosheleza katika
nyanja nyingi
Watakao hudhuria tamasha hilo watashuhudia kuzaliwa
upya kwa mwanamuziki wa kitanzania, Saida Karoli amabaye alirudi
katika tasnia ya muziki mwaka jana.
Ametaja baadhi ya wanamuki wanaotarajia kukonga nyoyo za
watazamaji katika tamasha hilo la 15 la sauti za busara ni pamoja na Zakes
Bantwini (Afrika Kusini), Kasai Allstars (DRC), Somi (Uganda/USA), Ribab Fusion
(Morocco), Kidum na tha boda boda band (Burundi/Kenya), Mlimani Park Orchestra
(Tanzani), Grace Matata (Tanzania) na Msafiri Zawose (Tanzania).
No comments:
Post a Comment