Msikie Humphrey Polepole kuhusu Ukawa...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi(CCM) Humphrey Polepole amedai kuwa kuanzishwa kwa Ukawa ilikuwa ni mpango mkakati wa Chadema kuvitumia vyama vingine.


Humphrey Polepole

Kupitia ukurasa wake wa Twitter Polepole amesema kuwa kwa sasa Ukawa haupo na kilichobaki ni Ukiwa.

Amesema “Hakuna kitu kinaitwa Ukawa, hii ilikuwa project ya Chadema ikivitumia vyama vingine, CUF, NCCR na NLD. Kilichobaki ni Ukiwa, katika jimbo lililokuwa la CUF leo CDM na CUF wanamenyana. Wazee wa Ufipa wala hawajali maana ni #WajasiramaliSiasa wale, Zindukeni.

Chimbuko la ukawa ilikuwa ni kipindi kile cha mchakato wa mabadiliko ya katiba. Hivyo baadhi ya vyama vya upinzani viliungana kwa madai kuwa ni kupigania maslahi ya wananchi kupitia Katiba mpya.

Vuguvugu hilo liliviunganisha vyama hivyo hadi kushirikiana katika uchaguzi wa wabunge, udiwani na urais mwaka 2015.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search