Simba wamkaribisha kocha mpya kibabe...soma habari kamili na matukio 360...#share

Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam

TIMU ya Simba imezidi kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi katika mbio za kuwania ubingwa wa ligi kuu ya Tanzania Bara ‘VPL’ baada ya kuitandika bila huruma timu ya singida united kwa magoli 4-0. Ushindi huo ni kama wamemkaribisha kocha wao mpya Mfaransa Pierre Lichantre kibabe

Baadhi ya wachezaji wa Simba wakishangilia moja ya goli.

Ushindi huo katika mchezo uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam umeifanya Simba kufikisha pointi 29 huku ikimuacha kwa pointi mbili Azama iliyoko nafasi ya pili ikiwa na pointi 27, baada ya jana kulazimishwa sare 1-1 na Majimaji ya Songea.

Alikuwa Shiza Ramadhani Kichuya alianza kuwanyanyua mashabiki wa Simba mnamo dakika ya 3 ya mchezo baada ya faulo ya Mwinyi Kazimoto uzembe wa mabeki wa Singida ulimpa mwanya mfungaji wa bao hilo.

Uzembe tena uliofanywa na mabeki wa Singida wakidhani kuwa Simba wameotea dakika ya 23 benki kisiki aliyesajiliwa toka Lipuli FC ,Asante Kwasi alifunga goli la pili huku likiwa la sita kwake na la kwanza akiwa na jezi ya Simba.

Akitokea benchi Mshambuliaji hatari mwenye kasi ya ajabu Emmanuel Okwi alifunga magoli mawili dakika ya 76 na 79 na kufikisha jumla ya magoli 10 akifutiwa na mshambuliaji wa Mbao FC mwenye magoli saba.


Kwa matokeo hayo pia Simba inamuacha mtani wake wa jadi klabu ya Yanga kwa pointi 7 kwani kwa sasa bYanga imejikusanyia pointi 22.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search