Sumatra kufungia mabasi yatakayochakachua mfumo wa VTS....soma habari kamili na matukio360..#share
Na mwandishi wetu, Mbeya
MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini(SUMATRA) mkoani Mbeya imeanza kufuatilia mienendo ya mabasi ya mikoani na itayafungia ikibaini kuvuruga (kuchakachua) mfumo wa kuratibu mwendo wa uendeshaji wa mabasi nchini (VTS).
Meneja wa Sumatra mkoani Mbeya, Denis Daudi
Meneja wa Sumatra mkoani Mbeya, Denis Daudi ameiambia matukio360 kuwa mabasi yatakayobainika kuchakachua mfumo huo hayatotozwa faini na yatafungiwa kutoa huduma ya usafirishaji.
Daudi amesema miaka ya nyuma serikali ilitumia gharama
kubwa za kuvunga vidhibiti mwendo lakini madereva walifanya uharibifu na kuendelea kukiuka sheria za usalama barabarani ikiwamo kuendesha kwa mwendo kasi na kuchangia ajari nyingi.
Amefafanua lengo la serikali kuweka mfumo huo ni kupungua
ajari za barabarani zinazogharimu maisha ya watanzania wengi na kwamba VTS ni maalum kwa kufuatilia mienendo ya madereva kuanzia mwanzo wa safari hadi mwisho.
Daudi amewaonya madereva kutofanya uharibifu katika mfumo na kwamba wazingatie sheria na kanuni mpya zilizowekwa na mamlaka hiyo na si vinginevyo na endapo wakienda kinyume zitawabana.
"Tumetoa elimu elekezi kwa wadau wa usafirishaji na kanuni mpya zilizowekwa na mamlaka, sasa isitokee tena mkikiuka na kuchukuliwa hatua mkalalamika,"amesema.
Pia ameonya wafanyabishara na waubiri wa dini kutoingia kwenye mabasi kwa lengo la kufanya biashara nakuhubiri kwa kuwa ni ukiukwaji wa sheria mpya zilizowekwa na mamlaka na endapo watabainika hatua za kisheria zitachukuliwa.
Meneja wa Sumatra mkoani Mbeya, Denis Daudi ameiambia matukio360 kuwa mabasi yatakayobainika kuchakachua mfumo huo hayatotozwa faini na yatafungiwa kutoa huduma ya usafirishaji.
Daudi amesema miaka ya nyuma serikali ilitumia gharama
kubwa za kuvunga vidhibiti mwendo lakini madereva walifanya uharibifu na kuendelea kukiuka sheria za usalama barabarani ikiwamo kuendesha kwa mwendo kasi na kuchangia ajari nyingi.
Amefafanua lengo la serikali kuweka mfumo huo ni kupungua
ajari za barabarani zinazogharimu maisha ya watanzania wengi na kwamba VTS ni maalum kwa kufuatilia mienendo ya madereva kuanzia mwanzo wa safari hadi mwisho.
Daudi amewaonya madereva kutofanya uharibifu katika mfumo na kwamba wazingatie sheria na kanuni mpya zilizowekwa na mamlaka hiyo na si vinginevyo na endapo wakienda kinyume zitawabana.
"Tumetoa elimu elekezi kwa wadau wa usafirishaji na kanuni mpya zilizowekwa na mamlaka, sasa isitokee tena mkikiuka na kuchukuliwa hatua mkalalamika,"amesema.
Pia ameonya wafanyabishara na waubiri wa dini kutoingia kwenye mabasi kwa lengo la kufanya biashara nakuhubiri kwa kuwa ni ukiukwaji wa sheria mpya zilizowekwa na mamlaka na endapo watabainika hatua za kisheria zitachukuliwa.
No comments:
Post a Comment