Taasisi ya moyo JKCI yaokoa milion 800....soma habari kamili na matukio360...#share
Na Abraham Ntambara,
Dar es Salaam
TAASISI ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa wiki moja imeokoa
sh.milioni 800 ambazo zingetumika kwenye upasuaji wa bila kufungua kifua (Catheterization) kwa watoto 15 wenye matatizo
ya moyo.
Katikati ni Mkurugenzi wa Matibabu ya Moyo wa JKCI Dk. Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Fedha hizo zingetumika kwenye upasuaji wa watoto hao kama
wangepelekwa nje ya nchi kwa matibabu.
Hayo yameelezwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa
Matibabu ya Moyo wa JKCI Dk. Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa habari
kuhusu upasuaji wa bila kufungua kifua kwa watoto hao.
Amesema upasuaji huo ulifanywa na taasisi hiyo kwa
kushirikiana na taasisi ya okoa moyo wa
watoto (save a child’s hesrt-sach) ya nchini Israel na kituo cha moyo cha
Berlin (Berlin Heart Center) cha nchini Ujermani.
“Upasuaji huu unatumia mtambo wa Cathlab umefanyika
katika kambi maalum ya matibabu iliyoanza Januari 20 hadi 25, 2018. Matibabu yaliyofanyika ni kuzibua matundu kwenye moyo
na kutanua mishipa ya moyo kwa watoto wenye umri wa kuanzia mwezi mmoja hadi
miaka 18,”
“Na kwa upasuaji huu tumeokoa sh. milioni 800 ambazo
zingetumika kama watoto hawa wangepelekwa kuhudumiwa nje,” amesema.
Dk. Kisenge amesema
kambi hiyo ilienda sambamba na uchunguzi wa moyo kwa watoto 32 ambapo watoto 20
watafanyiwa matibabu katika kambi hii na wengine 12 waliobaki watatibiwa na
madaktari wa JKCI kuanzia wiki ijayo.
Amesema kuwa wamepanga kufanya matibabu kwa watoto 20 na
wanaamini hadi kambi itakapomalizika watoto hao watakuwa wamepata matibabu.
Ameongeza kuwa kambi hiyo imeenda sambamba na utoaji wa elimu
ya upasuaji wa moyo wa bila kufungua kifua kwa watoto na jinsi ya kuwahudumia
watoto walipofanyiwa upasuaji huo.
Amewaomba wazazi na walezi kutosahau kupima afya za watoto
wao pale watakapoona kuna hali ya tofauti katika ukuaji wa watoto kwani
magonjwa mengi ya moyo yanaanzia utotoni.
Kwa upande wake Profesa wa Magonjwa ya Moyo kutoka kituo cha
moyo cha Berlin Protex Felix, amesema haoni sababu ya nchi kupeleka wagonjwe
kutibiwa nje kwani kunawataalamu wa ndani wanaoweza kufanya hivyo.
No comments:
Post a Comment