Yajue magonjwa yanayowasumbua wakazi Dar es salaam...soma habari kamili na matukio 360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

MGANGA Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dk. Grace Maghembe amesema magonjwa sugu yanayoongoza kuwaathiri wakazi wa jijini hapa ni kisukari, moyo na shinikozo la damu.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dk. Grace Maghembe akikata utepe kwenye uzinduzi wa kituo cha afya Aga Khan Ukonga jijini hapa.

Dk. Maghembe amesema hayo leo  alipokuwa akizindua kituo cha afya cha Aga Khan Ukonga jijini Dar es Salaam, amesema sababu ni tabia na mienendo ya wakazi kula vyakula vya wanga kwa wingi bila kufanya mazoezi.

“Takwimu za magonjwa yanayoongoza ni kisukari, moyo na shinikizo la damu, hutokana na mfumo wa maisha, tunakula vyakula vya wanga kwa wingi bila mazoezi hivyo vinabadilika kuwa mafuta,” amesema Dk. Maghembe.

Pia amesema kwa watoto wadogo wanaathiriwa zaidi na ugonjwa wa kifua.

Akizungumzia kituo cha afya kilichozinduliwa, amewapongeza Aga Khan kwa kusogeza huduma za afya nje ya mji na kuwaomba wapunguze gharama kwa wakazi wa eneo hilo ili waweze kupata huduma kwa gharama nafuu.

Amesema serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji katika sekta ya afya ili kufanikisha lengo la kuporesha huduma kwa wananchi kwani serikali serikali peke yake haiwezi kukidhi mahitaji.

Ameomba kituo hicho kusaidia katika kuhudumia wananchi wenye bima ya afya na ametoa wito kwa wananchi kujiunga na bima ya afya kwa ajili ya kupatiwa matibabu wakati wowote wanapohitaji.

Mkurugenzi Uendeshaji wa Vituo vya Afya Aga Khan Tanzania Fayyaz Taqi amesema kituo hicho kimegharimu sh.milioni 350 zilizotumika kwenye ukarabati wa jingo pamoja na vifaa tiba na maabara.

Amesema kuwa kitakuwa kikihudumia wagonjwa 100 hadi 150 kwa siku na kinakuwa kituo cha 9 kwa mkoa huu ambapo malengo yao ni kujenga vituo 10.

Ameongeza kuwa wameanzisha na kuendeleza mfumo wa afya jumuishi nchini ambao kwa pamoja na upanuzi wa hospitali kuu ya Aga Khan unaogharimu sh. bilioni 176 na unelenga kuongeza vitanda vya wagonjwa wa kulazwa, mafundisho na elimu ya tiba ya afya.

Ameeleza kwamba wanafanya hayo samamba na kukuza mtandao wa vituo 35 vya uhamasishaji nchini ambavyo vitachangia kuondokana na vikwazo visivyo muhimu vya upatikanaji wa huduma bora za afya ili kufikia kuleta athari chanya juu ya hali ya afya ya wananchi.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search