Ajifanya muuguzi na kuiba mtoto mchanga hospitalini.....soma habari kamili na

Na mwandishi wetu,Mbeya. 

POLISI mkoani Mbeya wanamsaka mwanamke aliyejifanya muuguzi na  kuiba  mtoto wa  kike  wa siku moja kwenye  wodi ya wazazi katika Hospitali  ya Mkoa , aliyezaliwa kwa njia ya upasuaji na Sarah Mwasanga(40) mkazi wa Iganzo jijini humo.
Kamanda Mohammed Mpinga


Kamanda wa Polisi  Mkoa wa Mbeya , Mohamed Mpinga amesema tukio hilo limetokea Februali 2, 2018  alfajiri   kabla ndugu na jamaa kuingia kuona wagonjwa.


Mpinga amesema  mwanamke huyo  alifika hospitalini hapo akiwa
kwenye usafiri wa pikipiki huku  amebeba kitu mithiri ya mtoto na
alipohojiwa na walinzi getini,  alieleza ana mgonjwa  ameandikiwa
sindano za saa na hivyo aliruhusiwa kuingia.

Mpinga amesema awali  alipoingia kwenye  wodi ya wazazi , aliwahoji
akinamama waliojifungua kuwa anahitaji mtoto wa kike kwa ajili ya
kumpatia chanjo , ndipo mzazi wa mtoto huyo alimkabidhi kwa kutambua
ni muuguzi kutokana na mavazi aliyokuwa amevaa.

Kamanda Mpiga amesema  hilo ni tukio kubwa lililotokea mkoani humo
 tangu aripoti  na kwamba wanaendelea na uchunguzi na kuomba wananchi
kutoa ushirikiano ili kufanikisha kupatikana kwa mtoto huyo.


Kaimu Mganga Mkuu , Yahaya Msuya , amekiri kutokea kwa tukio hilo, na
kwamba kwa sasa   lipo kwenye uchunguzi zaidi, na  limefikishwa katika
 kamati ya ulinzi na usalama .

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search