Magufuli awatunuku kamisheni maafisa 197 wapya JWTZ....soma habari kamili na matukio360....#share
Na mwandishi wetu, Dar es salaam
RAIS John Magufuli ambaye pia ni amir jeshi mkuu, leo Februari 3, 2018 amewatunuku kamisheni maafisa wapya 197 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Rais na Amir Jeshi mkuu wa Tanzania, Dk John Magufuli akitunuku kamisheni
Hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam na wamekuwa maafisa Luteni usu. Kati ya hao, wanawake ni 28.
Waliotunukiwa kamisheni ni maafisa wa Jeshi la JWTZ kutoka Tanzania na nchi marafiki waliopata mafunzo katika chuo cha mafunzo ya kijeshi Monduli mkoani Arusha
Kozi hiyo ilianza Januari, 2017 ikiwa na jumla ya wanajeshi 221 huku idadi ya wanajeshi kutokana nchi marafiki wakiwa ni 25. Miongoni mwa nchi hizo ni Uganda na Burundi.
Hii ni mara ya tano kwa rais Magufuli kutunuku kamisheni kwa wanajeshi wa JWTZ tangu aingie madarakani Novemba 2015
RAIS John Magufuli ambaye pia ni amir jeshi mkuu, leo Februari 3, 2018 amewatunuku kamisheni maafisa wapya 197 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Rais na Amir Jeshi mkuu wa Tanzania, Dk John Magufuli akitunuku kamisheni
Hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam na wamekuwa maafisa Luteni usu. Kati ya hao, wanawake ni 28.
Waliotunukiwa kamisheni ni maafisa wa Jeshi la JWTZ kutoka Tanzania na nchi marafiki waliopata mafunzo katika chuo cha mafunzo ya kijeshi Monduli mkoani Arusha
Kozi hiyo ilianza Januari, 2017 ikiwa na jumla ya wanajeshi 221 huku idadi ya wanajeshi kutokana nchi marafiki wakiwa ni 25. Miongoni mwa nchi hizo ni Uganda na Burundi.
Hii ni mara ya tano kwa rais Magufuli kutunuku kamisheni kwa wanajeshi wa JWTZ tangu aingie madarakani Novemba 2015
No comments:
Post a Comment