Chadema wamkataa msimamizi uchaguzi Kinondoni, waituhumu CCM kuingiza mamluki105...soma habari kamili na matukio360..share
Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam
CHAMA cha Chadema kimedai CCM imeleta mamluki zaidi ya 105 kutoka Zanzibar kuhujumu uchaguzi mdogo wa marudio wa ubunge Jimbo la Kinondoni utakaofanyika Februari 17, 2018
Pia Chadema imemkataa msimamizi wa uchaguzi jimbo la Kinondoni ikidai anaihujumu kwa makusudi.
Pia Chadema imemkataa msimamizi wa uchaguzi jimbo la Kinondoni ikidai anaihujumu kwa makusudi.
Mkuu wa Operesheni ya Uchaguzi wa Chadema Benson Kigaila akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu mwenendo wa uchaguzi Kinondoni.
Shutuma hizo zimetolewa leo jijini Dar es Salaam na Mkuu wa
Operesheni ya Uchaguzi wa chama hicho ,Bensoni Kigaila akizungumza na waandishi
wa habari kuhusu mwenendo wa uchaguzi huo.
“Tumebaini kwa nia mbaya Jumamosi Februari 4, 2018 majira ya
saa 4 asubuhi, CCM wameleta vijana kutoka Zanzibar kuja kufanya vurugu kwenye
uchaguzi wa Kinondoni,” amesema Kigaila.
Kigaila amedai watu hao wamegawanywa katika kambi tatu na wasambaziwa silaha aina ya panga, shoka na nondo.
Amedai vijana wa Chadema jana majira ya saa 9 Alasir walishuhudia gari aina ya Toyota Cruzer rangi ya Cream T ... DGS(namba tumezihifadhi) likiwa na watu 10 wakishusha silaha hizo kwenye ofisi za CCM zilizopo katika viwanja vya Alimapilau.
Amedai vijana wa Chadema jana majira ya saa 9 Alasir walishuhudia gari aina ya Toyota Cruzer rangi ya Cream T ... DGS(namba tumezihifadhi) likiwa na watu 10 wakishusha silaha hizo kwenye ofisi za CCM zilizopo katika viwanja vya Alimapilau.
Amesema vijana hao wa CCM wamehifadhiwa katika gesti na hoteli
mbalimbali zilizopo kinondoni huku akieleza kuwa baadhi wamehifadhiwa katika
gesti za kijitonyama, Mwananyamala na 80
wakiwa eneo la Vijana Magomeni.
Amesema kufuatia hali hiyo ni kwamba wamekwisha andika
barua ya kupeleka madai hayo kwa Inspekta Jenerali wa polisi (IGP) kwa ajili ya
kuchukua hatua ili fujo zisije kutokea.
Matukio360 ilimtafuta katibu wa Itikadi na uenezi wa CCM, Humphrey Polepole kuhusu tuhuma hizo, alijibu tuma ujumbe.
Alipotumiwa meseji hadi tunatoa habari hii hakujibu chochote.
Matukio360 ilimtafuta katibu wa Itikadi na uenezi wa CCM, Humphrey Polepole kuhusu tuhuma hizo, alijibu tuma ujumbe.
Alipotumiwa meseji hadi tunatoa habari hii hakujibu chochote.
Katika hatua nyingine Chadema imetangaza kumkataa msimamizi
wa uchaguzi wa Halmashauri ya Kinondoni kwa sababu kuu mbili.
Akitaja sababu hizo ni kwamba msimamizi huyo ameruhusu kwa
makusudi au kwa kujua kuruhusu tuhuma za kijinai dhidi ya Chadema zilizotolewa
na CCM kupelekwa kwenye kamati ya maadili kinyume na utaratibu.
Amesema katika tuhuma hizo ni kwamba CCM ilipeleka malalamiko
kuwa Chadema ilikiuka maadili ya Uchaguzi kwa vijana wanaodawa kuwa ni wa chama
hicho kumpiga kijana wa CCM huku ikijulikana kuwa swala hilo ni la jinai na
lilitakiwa kupelekwa polisi.
Na sababu nyingine ya kumkataa ni msimamizi huyo ambaye pia
ni Mkurugenzi wa halmashauri hiyo kwa makusudi ama kwa kutojua kuruhusu vikao
vya kamati ya maadili kusimamiwa na mwenyekiti asiyetambulika na wajumbe.
Hivyo kigaila amedai kutokana na sababu hizo wameona
kuwa kuna hujuma za makusudi zinafanywa na msimamizi huyo kwenye uchaguzi hivyo
kama akiachwa hawatafika salama.
No comments:
Post a Comment