Chadema wamvaa Magufuli,kuishtaki serikali...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

CHAMA cha Chadema kimemtaka rais John Magufuli kutoa kauli kuhusu watu 40 wanaoshikiliwa na jeshi la polisi kinyume na sheria ikiwa wanashikiliwa kwa agizo lake au la

Naibu katibu mkuu wa Chadema bara, John Mnyika 

Pia kimelitaka jeshi la polisi mapema leo kutoa dhamana au kuwafikisha mahakamani watu hao na endapo litashishindwa  kimedhamiria kuishtaki serikali ili mahakama iweze kutoa haki ya kuwapatia dhamana.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Bara, John Mnyika alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu watu 40 wanaoshikiliwana jeshi la polisi kutokana na maandamano ya chama hicho kwa siku sita mfululizo bila kupatiwa dhamana.

“Rais Magufuli ni vyema akatoa kauli na waziri wa mambo ya ndani atoe kauli iwapo uamuzi wa jeshi la polisi kuwashikilia watu wote hawa kinyume cha sheria mpaka hivi sasa  ni agizo lililotolewa na rais Magufuli au waziri wa mambo ya ndani,”

“Pia tunataka kauli kutoka kwa IGP, kamanda Mambosasa lakini vilevile tunahitaji kauli ya serikali kutoka kwa rais na kutoka kwa waziri wa mambo ya ndani ya nchi, na iwapo kauli hazitatolewa na serikali, iwapo jeshi la polisi halitawapa dhamana ama kuwafikisha mahakamani mapema kesho asubuhi, iwapo serikali haitatoa kauli inayostahili juu ya ukiukwaji huu wa sheria unaofanywa na jeshi la polisi sisi kama chama tunakusudia kuipeleka serikali mahakamani ili iweze kuwataka iwape dhamana,” amesema Mnyika.

Mnyika amesema watu hao wanashikiliwa katika kituo cha kati “Central”, Msimbazi na  Ostabey.

Naibu katibu huyo amesema miongoni mwa watu hao wawili wana majeraha ya risasi na hawajapatiwa matibabu yanayostahili lakini pia kuna mzazi anayenyonyesha mtoto wa miezi minne aliyeko katika kituo cha kati pamoja na kijana wa miaka 15 mwanafunzi.




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search