Huduma ya afya sasa kutolewa kielektroniki....soma habari kamili na matukio360..#share

Na Salha Mohamed, Dar es Salaam

WIZARA ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto inatarajia kukusanya na kutumia takwimu kwa njia ya kielektroniki nchini  ili  kutoa huduma za afya kwa ubora.

Dk Mpoki Ulisubisya

Hayo yameelezwa leo  jijini  Dar es Salaam  na katibu mkuu wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia ,wazee na watoto Dk. Mpoki Ulisubisya wakati wa  kuweka sahihi ya makubaliano ya kuanzisha mfumo wa ukusanyaji takwimu za afya utakaotekelezwa na Wizara ya afya,Wadau wa Maendeleo,Asasi za Kiraia na Shirika la Afya Duniani (WHO).

“Takwimu ni muhimu zitamuwezesha mtoa huduma kujua  historia ya ugonjwa wa  mgonjwa  na matibabu aliyopewa awali,kuwapa uwezo utumishi kujua tunahitaji rasilimali watu kwa kiasi gani  katika kituo cha Afya,” amesema Dk. Ulisubsya.

Dk. Ulisubisya amesema kwa kuanzia mchakato huo  utaanza kwenye mikoa ya Tanga,Kilimanjaro na Manyara  na hadi kufikia  2020  utakamilika mikoa yote.

Amesema mfumo wa kujaza takwimu kwenye makaratasi umepitwa na wakati na kadri makaratasi ya takwimu yanapokuwa mengi, makosa ya utoaji huduma yanatokea.


Katika hatua nyingine Dk. Ulisubisya amesema hadi sasa hali ya utoaji  chanjo imefikia asilimia 97 na lengo ni kufika asilimia 100 kupitia mfumo huu wa kukusanya takwimu kwa njia ya kielektroniki.

Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dk. Matthieu Kamwa amesema  wapo  tayari kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Afya katika kutekeleza hilo ili kuweza kuboresha mifumo ya afya nchini.

“Unajua Takwimu ni utajiri hasa katika kutekeleza shughuli za kutoa huduma za afya kwa wananchi hivyo hatuna budi kuunga mkono juhudu za Serikali ya Tanzania katika kufanikisha hili jambo  litaturahisishia hata sisi katika kutoa miongozo ya afya,” amesema Dk. Kamwa.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search