CHADEMA:Kuna njama za kumkamata mgombea ubunge wetu ...soma habari kamili na matukio360..#share
Na Abraham Ntambara,
Dar es Salaam
CHAMA cha Chadema kimedai kuna mpango maalum wa kukamatwa kwa mgombea ubunge wa chama hicho jimbo la Siha, Elvis Mossi na kumuweka mahabusu hadi uchaguzi utakapomalizika.
Pia chama hicho kimeshangazwa na wakuu wa mikoa na wilaya kujihusisha katika kampeni za uchaguzi wakati Nec iliwaandikia barua viongozi hao ikiwazuhia kushiriki kwenye kampeni.
Dk Vicent Mashinji
Akizungumza na
waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam katibu mkuu wa Chadema, Dk Vicent Mashinji amedai taarifa walizonazo ni kuwa mpango huo utaongozwa na mkuu wa wilaya ya Siha, Onesmo Buswilu.
Pia kimelaani kitendo cha askari polisi waliokuwepo katika eneo la tukio kushindwa kulichukulia suala hilo kwa umakani unaohitajika.
"Taarifa tulizonazo kuna mpango maalum wa kumkamata na kumuweka mahabusu mgombea wetu wa ubunge jimbo la Siha hadi uchaguzi umalizike. Utaratibiwa na mkuu wa wilaya ya Siha, Onesmo Buswilu,'' amesema Mashiji na kuongeza ''Ajabu nyingine ni kuwa pamoja na Nec kuwapiga marufuku wakuu wa mikoa na wilaya kushiriki katika uchaguzi, viongozi hao wanaendelea kuwanadi wangombea wa chama chao."
"Kwa kuwa NEC ni chombo huru kihakikishe kinasimamia uchaguzi huu kwa uhuru na haki,'' amesema.
Katika hatua nyingine chama hicho kimelaani kitendo cha mgombea wao wa udiwani kata ya Guhangaza wilayani Muleba mkoani Kagera, Mchungaji Athanas Makoti kutekwa, kuteswa, kunyanyaswa, kuonewa na kulazimishwa kujitoa kugombea nafasi hiyo.
Pia kimelaani kitendo cha askari polisi waliokuwepo katika eneo la tukio kushindwa kulichukulia suala hilo kwa umakani unaohitajika.
“Hiki ni kitendo
ambacho hakikubaliki, ninaimani hata huku kuumizwa alikonako kwa sasa huenda
wangeliwahi huyu mgombea wetu asingeumia kwa kiasi hiki alichoumia kwa hivi
sasa,” amesema Dk Mashinji.
Amesema kwa mujibu wa
ushuhuda wa mgombea huyo na watu wengine hawana shaka kuwa tukio hilo ni njama za kisiasa zenye uhusiano na uchaguzi wa marudio katika
kata ya Guhangaza, wilayni Muleba, mkoani Kagera.
Amesema taarifa walizonazo ni kwamba hospitali aliyokuwa akipatiwa matibabu
imempa rufaa akapate matibabu zaidi na kueleza hali hiyo inaonesha ni kwa kiasi kikubwa meumizwa.
Dk Mashinji amelitaka
jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa haraka dhidi ya kitendo hicho na kutoa taarifa mapema ili aliyehusika afikishwe kwenye vyombo vya sheria.
No comments:
Post a Comment