John Bocco mchezaji bora mwezi Januari.... soma habari kamili na matukio360....#share
Na
Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
NAHODHA
wa timu ya Simba, John Bocco amechaguliwa
kuwa mchezaji bora wa mwezi Januari ,2018 wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL)Tanzania Bara.
John Bocco aliyevaa jezi nyekundu akimiliki mpira katika moja ya mechi ya ligi kuu Tanzania Bara.
Mshambuliaji
huyo ametwaa tuzo hiyo baada ya kuwashinda Emmanuel Okwi wa Simba na Awesu
Awesu wa Mwadui kutokana na uchambuzi uliofanywa na Kamati ya Tuzo za VPL
zinazotolewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana wiki
hii kupitia ripoti za makocha kutoka viwanja mbalimbali ambavyo ligi hiyo
inachezwa.
Bocco alitoa
mchango mkubwa kwa Simba mwezi huo ikipata pointi tisa katika michezo mitatu
iliyocheza na kuendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi, huku mshambuliaji
huyo akifunga mabao matatu na kutoa pasi mbili za usaidizi wa bao.
Pia
kiwango cha mshambuliaji huyo aliyecheza dakika zote 270 za michezo mitatu ya
Simba mwezi huo kilikuwa juu karibu kila mchezo.
Kwa
upande wa Okwi aliyecheza dakika 206 kati ya 270 ilizocheza timu yake, alitoa
mchango mkubwa kwa Simba kupata idadi hiyo ya pointi na kuendelea kubaki
kileleni mwa msimamo wa ligi, huku akifunga mabao manne. Simba iliifunga
Singida United mabao 4-0,ikaifunga Kagera Sugar mabao 2-0 na kisha ikailaza
Majimaji mabao 4-0.
Awesu
aliingia katika hatua hiyo kutokana na kung’ara katika michezo ambayo Mwadui
ilicheza mwezi huo, akiibuka Mchezaji Bora katika mchezo wao dhidi ya Yanga,
Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam uliomalizika kwa timu hizo kutofungana, pia
aliibuka mchezaji bora wa mchezo wo dhidi ya Njombe uliofanyika Uwanja wa
Mwadui, Shinyanga na timu hizo kufungana mabao 2-2.
Mshambuliaji huyo aliyecheza kwa dakika 322 kati ya 360 ilizocheza Mwadui alifunga bao moja na kuisaidia timu yake kupata pointi sita katika mechi nne ilizocheza mwezi huo, ikitoka sare tatu na kushinda moja, ikiendelea kubaki nafasi ya kumi.
Mshambuliaji huyo aliyecheza kwa dakika 322 kati ya 360 ilizocheza Mwadui alifunga bao moja na kuisaidia timu yake kupata pointi sita katika mechi nne ilizocheza mwezi huo, ikitoka sare tatu na kushinda moja, ikiendelea kubaki nafasi ya kumi.
Kutokana
na ushindi huo, Bocco atazawadiwa tuzo, kisimbuzi cha Azam na fedha taslimu sh.
milioni moja kutoka kwa Mdhamini Mkuu wa Ligi, Kampuni ya Vodacom
Tanzania.
Wachezaji wengine ambao tayari wameshinda Tuzo ya Mchezaji Bora wa mwezi wa VPL msimu huu na miezi yao katika mabano ni Okwi (Agosti), beki wa Singida United, Shafiq Batambuze (Septemba) na mshambuliaji wa Yanga, Obrey Chirwa (Oktoba).
Wachezaji wengine ambao tayari wameshinda Tuzo ya Mchezaji Bora wa mwezi wa VPL msimu huu na miezi yao katika mabano ni Okwi (Agosti), beki wa Singida United, Shafiq Batambuze (Septemba) na mshambuliaji wa Yanga, Obrey Chirwa (Oktoba).
Wengine
ni kiungo wa Singida United, Mudathir Yahya (Novemba) na mshambuliaji wa Mbao
FC ya Mwanza, Habibu Kiyombo (Desemba).
No comments:
Post a Comment