Mbunge Mwakajoka awekwa mahabusu....soma habari kamili na matukio360...#share
Na mwandishi wetu, Tunduma
MBUNGE wa Tunduma, wilayani Momba mkoani Songwe(Chadema), Frank Mwakajoka amekamatwa na polisi kisha kuwekwa mahabasu kwa saa 48 Kwa kinachodaiwa ni amri ya mkuu wa wiilaya hiyo, Jumaa Irando
Hatua hiyo inadaiwa ni mbunge huyo kuwahamasisha wananchi wasichangie michango ya ujenzi wa zahanati moja kwa kuwa tayari serikali imetenga fedha za ujenzi huo.
Frank Mwakajoka
Mwakajoka amekamatwa akiwa njiani akienda katika shughuli zake baada ya kuhudhuria kikao cha madiwani.
Hii ni mara ya pili kwa Mbunge Mwakajoka kukamatwa na kuwekwa mahabusu kwa saa 48 kwa amri ya mkuu huyo wa wilaya. Agosti mwaka jana Irando aliamuru kukamatwa Mwakajoka kwa kile alichodai alitoa lugha ya kumdhalilisha yeye na Serikali ya Mkoa wa Songwe wakati akiwa kwenye mkutano wa hadhara.
MBUNGE wa Tunduma, wilayani Momba mkoani Songwe(Chadema), Frank Mwakajoka amekamatwa na polisi kisha kuwekwa mahabasu kwa saa 48 Kwa kinachodaiwa ni amri ya mkuu wa wiilaya hiyo, Jumaa Irando
Hatua hiyo inadaiwa ni mbunge huyo kuwahamasisha wananchi wasichangie michango ya ujenzi wa zahanati moja kwa kuwa tayari serikali imetenga fedha za ujenzi huo.
Frank Mwakajoka
Mwakajoka amekamatwa akiwa njiani akienda katika shughuli zake baada ya kuhudhuria kikao cha madiwani.
Hii ni mara ya pili kwa Mbunge Mwakajoka kukamatwa na kuwekwa mahabusu kwa saa 48 kwa amri ya mkuu huyo wa wilaya. Agosti mwaka jana Irando aliamuru kukamatwa Mwakajoka kwa kile alichodai alitoa lugha ya kumdhalilisha yeye na Serikali ya Mkoa wa Songwe wakati akiwa kwenye mkutano wa hadhara.




No comments:
Post a Comment