Profesa Bisanda awaasa vijana nchini....soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

VIJANA wametakiwa kuwa na fikra, mtazamo chanya kwenye uwajibikaji ili kutambua nafasi waliyonayo katika kutumia fursa zilizopo nchini ili kujiletea maendeleo.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria, Profesa Elifas Bisanda (kulia) na Mkurugenzi wa IYF Profesa Seong Hun Kim (kushoto) wakisaini makubaliano ya utoaji  elimu ya kubadili fikra kwa wanafunzi wa chuo hicho.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Profesa Elifas Bisanda wakati wa utilianaji saini makubaliano ya ushirikiano baini ya chuo hicho na IYF (International Youth Fellowship) kutoka Korea Kusini kwa ajili ya kutoa elimu ya kubadili fikra kwa wanafunzi.

“Tunahitaji vijana wa taifa hili waanze kuwajibika na kutambua  kwamba wananafasi kubwa ya kuleta maendeleo pale walipo kwa kutumia fursa zilizopo,” amesema Prof. Bisanda.

“Haiwezekani nchi kama Tanzania ambayo bado inaardhi kubwa isiyo na watu, inayofaa kwa kilimo, ufugaji na utalii lakini vijana wanakimbilia mijini ambako hakuna kazi,” ameongeza.

Akizungumzia kuhusu makubaliano hayo, Profesa Bisanda amesema IYF itasaidia kuleta walimu nchini watakaofundisha  elimu  ya kubadili fikra.

Amesema faida ya elimu hiyo inasaidi kufanya mambo katika maisha kwa utaratibu, lakini pia inamfanya mtu kujua umuhimu wa kuwajibika katika kujishughulisha na masuala ambayo yatamsaidia binafsi na jamii.

“Leo hii katika nchi yetu tuna tatizo la ajira, vijana wengi wakimaliza vyuo wanakaa tu, wanasema tunasubiri kupata kazi, lakini si hivyo katika nchi zingine, vijana wa leo wanachagua kazi, hivyo mawazo tuliyonayo watanzania inatakiwa fikra zibadilike, inatakiwa kujifunza maarifa mapya na mbadala,” amesema.

Mkurugenzi wa IYF Profesa Seong Hun Kim, amesema  wanafunzi wa chuo kikuu Huria cha Tanzania pia watapata fursa ya kushiriki katika kambi za vijana za kimataifa zinazofanyika kila mwaka  mwezi Julai.


“Sisi tulianza kuwekeza katika kulea watu na pia kufanya kampeni kupitia serikali kuhusu mabadiliko ya fikra na mitazamo yao. Kupitia mafanikio na uzoefu wa Korea Kusini  unaweza kusaidia Tanzania kwa kupitia mikutano na makongamano mbalimbali,” amesema Prof. Kim.






About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search