Samia awataka skauti kushiriki shughuli za uzalishaji mali...soma habari kamili na matukio360...share


Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MAKAMU wa rais Samia Suluhu Hassan amewataka Skauti nchini Tanzania kushiriki katika shughuli za Uzalishaji mali kwa lengo la kujiongezea kipato na kukabiliana na changamoto ya Ukosefu wa Ajira hasa kwa Vijana.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi,Vijana na Ajira Anthony Mavunde akifungua mkutano mkuu wa Skauti Tanzania mjini Dodoma.

Hayo yamesemwa leo Mkoani Dodoma katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Skauti Nchini ambapo akisoma hotuba ya makamu wa rais  Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi,Vijana na Ajira Anthony Mavunde ambaye alikuwa mgeni rasmi.

Katika hotuba hiyo, makamu wa rais  amewapongeza skauti kwa kushiriki katika matukio ya kijamii ikiwemo wakati wa maafa Kilosa na Pugu kwenye machimbo.

Aidha amewataka skauti kuwa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba Amani na Mshikamano wa nchi unalindwa kwa nguvu zote.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi, makamu wa rais wa Skauti Tanzania Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakary Zubeiry amebainisha mipango mbalimbali ya Skauti Tanzania katika kujiletea maendeleo na pia amemhakikishia mgeni rasmi kwamba Skauti Tanzania itaendelea kujikita katika kusimamia HAKI, USAWA na UZALENDO pamoja na kuhimiza AMANI na  MSHIKAMANO miongoni mwa Watanzania.

Mkutano huo mkuu wa skauti agenda yake kuu ni Uchaguzi wa Uongozi wa Skauti na Wajumbe wa Bodi.

Kwasasa sasa Skauti Tanzania ipo chini ya Uongozi wa Skauti Mkuu Mama Mwantumu Mahiza na Kamishna Mkuu Abdulkarim Esmail Shah.




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search