Tetesi za soka Ulaya leo Jumatatu....soma habari kamili na matukio360....#share

Na mashirika ya kimataifa
Chelsea wanaangalia uwezekano wa kumfuta kazi, Antonio Conte na mahala pake kumleta aliyekuwa meneja wa Watford, Marco Silva katika mkataba wa muda. (Times)
Antonio Conte
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho anataka kuwashinda Manchester City katika kumsaini kiungo wa kati wa Real Madrid Isco. (Star)
Real Madird watamwendea kipa wa Chelsea Thibaut Courtois, 25, baada ya kuamua kuwa itakuwa rahisi kumsaini kuliko Mhispania mweye umri wa miaka 27 David de Gea kutoka Manchester United. (Talksport)
Mlinzi wa Tottenham Toby Alderweireld hawezi kusafiri kwenda Turin kwa mechi ya ligi ya mabingwa na Juventus halia ambayo inaweka hamtma yake katika klabu hiyo kuwa yenye utata.
Mshambuliaji wa Uhispania Fernando Llorente, 32, ametilia shaka hatma yake huko Tottenham akikiri kuwa ameokosa Juventus. (Mirror)
Kocha wa Chelsea Antonio Conte anasema wachezaji wake hawaathiriki kwa vyoyote na uvumi unazunguka hatma yake klabuni. (Sky Sports)
Beki wa Real Madrid Marcelo anaamini kuwa mshambuliaji wa Paris St-Germain Neymar, 26, atajiunga na klabu hiyo siku za usoni na anaamini kuwa ikiwa mbrazil huyo mwenzake atakuwa bora kwa klabu hiyo ya La Liga. (Marca)
Lakini beki wa PSG Thiago Silva anaamini kuwa Neymar atasalia katika klabu hiyo. (Canal+ via Goal)
Meneja wa West Brom Alan Pardew anatepeleka kikosi chake nchini Uhispani kwenye joyo kwa mazoezi wakati wanajaribu kuzuiz kuondolewa kutoka kwa Ligi. (Telegraph)

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search