Zitto ataka mkutano wa maridhiano...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Arusha

KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe ametaka kuitishwa kwa mkutano wa kitaifa wa maridhiano ya kisiasa nchini.

Kiongozi wa Chama cha ACT wazalendo, Zitto Kabwe akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha jana,kuhusu hali ya kisiasa nchini na matukio ya kihalifu yanayoendelea kutokea. 





Amesema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, amesema mkutano huo utalenga kujadili changamoto zote za uendeshaji wa siasa nchini na kukubaliana kanuni za demokrasia ya vyama vingi.

"Hii ni kutokana na dhahiri kwamba mfumo wa vyama vingi nchini upo hatarini zaidi kuliko wakati wowote," amesema Zitto.

Zitto amesema wadau wanaoweza kufanikisha mkutano huo ni asasi za kiraia, vyama vya wafanyakazi, vyama vya wafanyabiashara, na vyama vya wakulima na wafugaji.

Amesema hali ya kisiasa ya sasa nchini siyo ya kuachia wanasiasa peke yake maana sasa inahusu uhai wa watu na wengine wasio jihusisha na siasa.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search