Zuma aomba kuongezewa miezi mitatu hadi sita..soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mashirika ya Kimataifa
RAIS wa Afrika Kusini, Jacob  Zuma ameomba kuongezewa muda wa kati ya miezi mitatu hadi sita ili  ajiuzulu kwa hiari yake.
Rais Jacob Zuma
Hatua yake hiyo inafuatia kuwapo kwa shinikizo la ndani na nje ya chama chake cha ANC ambapo kimemtaka rasmi rais huyo ajiuzulu baada ya kukataa kufanya hivyo mapema hii leo.
Hakujatolewa muda wa mwisho kwake kuondoka madarakani, lakini imebainika kuwa mrithi wake atakuwa Cyril Ramaphosa ambaye ni rais wa chama cha ANC.
Hatua hii ya ANC inaonekana ndio njia rahisi zaidi ya chama hicho kumng'oa rais Zuma madarakani badala ya kusubiri utaratibu wa bunge ambao ungeweza kuwa mrefu na wenye madhara zaidi kwa chama cha ANC.
Rais Zuma ambaye anakabiliwa na mashtaka kadhaa ya rushwa, alishindwa uongozi wa chama tawala Desemba mwaka jana.
Kiongozi mpya wa ANC, Cyril Ramaphosa anaongoza shinikizo za kumuondoa Zuma katika nafasi yake hiyo ya Urais, na hatimaye kushika pia nafasi hiyo.
Ramaphosa ameahidi pia kupambana na rushwa iliyokithiri na kukijenga upya chama cha ANC, wakati nchi hiyo ikielekea katika uchaguzi mwakani.
Iwapo Bwana Zuma, mwenye umri wa miaka 75, hatotekeleka, atakabiliwana kura ya kutokuwa na imani naye bungeni ambayo anatarajiwa kushindwa.
Akiwa amehudumu madarakani tangu 2009, ameandamwa kwa tuhuma za rushwa.
Chama cha ANC hakijathibitisha rasmi mipango yake lakini duru kutoka cham hicho zimetoa ufafanuzi katika vyombo vya habari nchini Afrika kusini na pia kwa shirika la habara la kimataifa la Reuters.
Rais Zuma amekiuka shinikizo linaloongezeka la kumtaka ajiuzulu tangu Desemba wakati Cyril Ramaphosa alipoichukua nafasi yake kama kiongozi wa chama cha ANC.
Katibu mkuu wa ANC, Ace Magashule ameiwasilisha barua kwa kiongozi huyo anayepigwa vita nyumbani kwake katika mji mkuu Pretoria, na kumuarifu rasmi kuhusu uamuzi wa chama hicho wa kumtaka aondoke katika mkutano na kamati ya kitaifa ya utendaji (NEC), taarifa zinasema.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search