Apandishwa kortini akituhumiwa kusafirisha gramu 214 za heroine...soma habari kamili na matukio360....#share



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imempandisha kizimbani Mfanyabiashara, Hariri Mohammed Hariri (45), mkazi wa Kinondoni jijini Dar es Salaam, kujibu Tuhuma za kusafirisha zaidi ya gramu 214 za dawa za kulevya.
Mfanyabiashara, Hariri Mohammed Hariri (45) akiwa ameambatana na askari polisi katika viunga vya mahakama ya hakimu mkazi kisutu jijini Dar es Salaam.

Akisoma hati ya mashtaka Wakili wa serikali, Clara Chalwe mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi inadaiwa Machi 2 mwaka huu huko Kinondoni Matitu ndani ya Wilaya ya Kinondoni mshtakiwa alisafirisha dawa za kulevya aina ya Heroine Hydrochloride zenye uzito wa gramu 214.11.

Hata hivyo, mshtakiwa hakuruhusiwa kujibu chochote mahakamani  kwa kuwa Mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi za dawa za kulevy isipokuwa kwa kibali kutoka kwa DPP.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka, upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika. Na imeahirishwa hadi Aprili 4 mwaka huu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search