Waziri Mwakyembe amuonya Diamond.... soma habari kamili na matukio360...#share
Na mwandishi wetu, Dar es salaam
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dk Harrison Mwakyembe amemtaka msanii wa muziki Nassib Abdul ' Diamond Platinum' aache kulumbana na serikali
Dk Harrison Mwakyembe
Anaandika Mwakyembe;
Begin forwarded message:
From: Harrison George Mwakyembe <mwakyembe.harrison@gmail.com>
Date: March 20, 2018 at 6:31:41 PM GMT+3
To: solomonmwansele@gmail.com
Subject: Diamond
Nimesikitishwa sana na matamshi ya mwanamziki Diamond wakati akihojiwa na mtangazaji wa Times FM, Lil Ommy, kwa hatua ambazo Wizara inachukua kulinda maadili ya Kitanzania katika tasnia ya sanaa.
Maamuzi ya kuzifungia baadhi ya nyimbo na wasanii wawili kwa kukiuka maadili, yalifanywa kwa mujibu wa sheria na si kwa utashi binafsi wa Mhe. Naibu Waziri anayemlaumu. Diamond atambue kuwa Serikali ina taratibu zake. Maamuzi ya Naibu Waziri ni maamuzi ya Wizara.
Kama ni vikao na wasanii, tumefanya vingi sana, lakini Diamond hahudhurii vikao hivyo na si wajibu wa Serikali kumfanyia kikao chake mwenyewe, however popular he is. Hatuwezi kuwa na sheria kwa wasanii wengine na sheria maalum kwake, nadhani hizi ni dalili za kuanza kulewa umaarufu kwani Diamond si Kiongozi wa Shirikisho la Muziki wala msemaji wa Chama cha Muziki wa kizazi kipya kuwasemea wenzake.
Si busara kwake kushindana na Serikali, na kama ana ushauri basi autoe kistaarabu utazingatiwa lakini si kwa kumshambulia Naibu Waziri kwa dharau na kejeli jinsi alivyofanya. Sijafurahishwa hata kidogo.
No comments:
Post a Comment