Bavicha wapinga maamuzi ya waziri....soma habari kamili na matukio360...#share
Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam
BARAZA la Vijana wa Chadema(Bavicha) limepinga hatua ya Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo Juliana Shonza kumfungia msanii Ibrahim Mussa “Roma Mkatoliki”
kujihusisha na muziki kwa miezi sita.
Mwenyekiti wa barza la vijana Chadema (Bavicha) Patrich Ole Sosopi akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Juzi Naibu waziri huyo alitangaza uamuzi huo dhidi ya msanii
huyo kwa madai kuwa ameshindwa kufanya baadhi ya marekebisho aliyotakiwa
kufanya kwenye wimbo wake wa “kibamia”
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,
Mwenyekiti wa Bavicha, Patrick Ole Sosopi amesema naibu waziri huyo hana mamlaka
hiyo bali wenye mamlaka ya kufanya hivyo ni Baraza na Sanaa nchini (Basata).
“Tumesikitishwa sana kama baraza na kama chama, tunaona
kwamba serikali hii inahamasisha watu wajiajiri, kama mtu amekosea na kama
wimbo ni mbaya ni kwa nini wasiweze kusimamisha wimbo mmoja,
tunaona kabisa kuna sura ya kisiasa na tunalaani kitendo hiki,” amesema Ole
Sosopi.
“Roma Mkatoliki tumeona wakati mwingi akiendelea kuimba
nyimbo za kiharakati na kiukombozi katika nchi hii na nyimbo zake nyingi
zimekuwa zikionesha namna ya kukosoa serikali, naibu waziri hana mamlaka hayo
ya kumfungia msanii bali ni Basata,” amesema Ole Sosopi.
Amesema Basata imeshindwa kufanya kazi yake kwa umakini
na kuonesha kuwa linafanya kazi kwa maelekezo na kama wangekuwa makini na
kufanya kazi kwa mujibu wa taratibu na sheria walipaswa kufungia nyimbo mapema baada ya kutoka.
Ole Sosopi amesema kumfungia na kokaa bila kufanya kazi yake ni
sawa na kitendo cha mauaji kwa sababu anasomesha, anategemewa na ndugu hivyo
kumfungia kwa kipindi hicho maana yake asile, asisomeshe na kusimama katika
maisha yake ya kawaida na kumfanya aidha awe kibaka ama mwizi.
Amesema kutokana na jambo hilo kama baraza litampa Roma
msaada wa kisheria kwa kumpatia wakili atakayemsaidia kufungua shauri
mahakamani ili kudai haki yake.
No comments:
Post a Comment