Jinsi moto ulivyoteketeza soko la mbagala....soma habari kamili na matukio360...#share
Na Salha Mohamed, Dar es Salaam
SOKO la Mbagala rangi tatu wilayani Temeke jijini Dar es salaam leo limeteketea kwa moto na kusababisha hasara kwa zaidi ya wafanyabiashara 300 hasa wauza nguo za mitumba.
Moto huo ulioanza asubuhi chanzo chake hakijajulikana hadi sasa ikiwa ni miezi kadhaa tangu kuungua kwa soko hilo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke, Emmanuel Lukula amethibitisha kuungua kwa soko hilo na kwamba hakuna madhara ya kifo yaliyotokea.
Kamanda Lukula amesema moto huo umeteketeza soko hilo kwa saa tatu ña kwamba ulianza majira ya saa moja asubuhi.
"Nilifika eneo la soko saa 1 lakini niliukuta moto ukiwa mkubwa sana nikawasiliana na kikosi cha zimamoto na kufanikiwa kuudhibiti moto huo kwa saa tatu," amesema na kuongeza chanzo cha moto huo bado hakijajulikana.
Amesema baada ya kufanikiwa kuuzima moto huo kamati ya maafa ya Kata hiyo imekaa kwa ajili ya kutathmini watu waliounguliwa pamoja na bidhaa zilizoungua.
Amesema kamati ikimaliza kutathmini watampelekea na kuitoa hadharani
SOKO la Mbagala rangi tatu wilayani Temeke jijini Dar es salaam leo limeteketea kwa moto na kusababisha hasara kwa zaidi ya wafanyabiashara 300 hasa wauza nguo za mitumba.
Moto huo ulioanza asubuhi chanzo chake hakijajulikana hadi sasa ikiwa ni miezi kadhaa tangu kuungua kwa soko hilo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke, Emmanuel Lukula amethibitisha kuungua kwa soko hilo na kwamba hakuna madhara ya kifo yaliyotokea.
Kamanda Lukula amesema moto huo umeteketeza soko hilo kwa saa tatu ña kwamba ulianza majira ya saa moja asubuhi.
"Nilifika eneo la soko saa 1 lakini niliukuta moto ukiwa mkubwa sana nikawasiliana na kikosi cha zimamoto na kufanikiwa kuudhibiti moto huo kwa saa tatu," amesema na kuongeza chanzo cha moto huo bado hakijajulikana.
Amesema baada ya kufanikiwa kuuzima moto huo kamati ya maafa ya Kata hiyo imekaa kwa ajili ya kutathmini watu waliounguliwa pamoja na bidhaa zilizoungua.
Amesema kamati ikimaliza kutathmini watampelekea na kuitoa hadharani
No comments:
Post a Comment