Majaliwa: Wafanyabiashara tumieni taasisi za kifedha kukopa...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Ruangwa


WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amewataka wafanyabiashara wilayani Ruangwa kutumia taasisi za kifedha kukopa fedha kwa ajili ya kukuza mitaji yao.

Kassim Majaliwa

Ameyasema hayo leo (Jumapili, Machi 25, 2018) wakati akizungumza na wafanyabiashara wa wilaya hiyo katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Chama Cha Walimu, wilayani Ruangwa.

Waziri Mkuu ambaye yuko wilayani Ruangwa kwa ziara ya kikazi ya siku mbili amesema ni vema wakatumia taasisi za kifedha zilizopo ili kukuza mitaji yao.

”Naamini sekta ya biashara ni muhimu katika mabadiliko ya maendeleo, hivyo wafanyabiashara ni chachu ya maendeleo kokote na Serikali itaendelea kuwaunga mkono.”

Amesema katika kuhakikisha riba zinapungua, Rais John Magufuli anaendelea kuzungumza na wamiliki wa taasisi za kifedha ili waone namna ya kupunguza riba hiyo.

Waziri Mkuu amesema lengo la Serikali la kuchukua hatua hiyo ni katika kutekeleza mkakati wake wa  kuwawezesha wafanyabiashara ili waweze kupata mikopo yenye riba nafuu.

Pia Waziri Mkuu amewahakikishia wananchi wa wilaya hiyo kwamba Serikali ipo pamoja nao na imedhamilia kuboresha huduma mbalimbali za jamii kama maji na afya.

Naye, Mwenyekiti wa Umoja wa Wafanyabiashara wa Wilaya ya Ruangwa, Said Shea amewaomba wafanyabiashara wenzake watumie fursa za maendeleo zilizoko wilayani humo kwa kupanua wigo wa biashara zao.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search