Warami watoa ya mayoni kwa maaskofu...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaama

WATETEZI wa Rasilimali Wasio na Mipaka (Warami) wemeshauri Maaskofu kujikita kwenye masuala mahususi yanayohusu dini katika kuelimisha na kumuachia kaisali yaliyo yake na ya Mungu yaliyo yake.
Mkurugenzi wa Utafiti Warami Philipo Mwakibinga, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam.

Ushauri huo umekuja siku moja baada ya kusambaa kwa ujumbe wa pasaka kutoka baraza la maaskofu wa Kanisa la Kilutheri Tanzania (KKKT) na kusainiwa na maaskofu 27 ukizungumzia masuala mbalimbali ya kijamii, kisiasa, kiuchumi kwa kukosoa na kushauri huku ukiitaka serikali kuchukua hatua hususani suala la katiba mpya.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Utafiti Warami Philipo Mwakibinga, amesema viongozi wa dini wana wajibu wa kiutumishi katika jamii huku wakilinda dhamira yao ya kuhakikisha umoja wa nchi unabaki kuwa salama kwa namna yoyote ile.

“Jana tuliona katika mitandao ya kijamii waraka wa viongozi wetu wa dini, ukizungumzia masuala mbali mbali ya nchi na mwelekeo wake huku sehemu kubwa ya waraka huo ukijikita katika kuikosoa serikali juu ya namna inavyoendeshwa,” amesema Mwakibinga.

Ameongeza “Tunatoa wito kwa Maaskofu wetu kujikita katika masuala mahususi yanayohusu dini, watuelimishe kwenye dini, wamuachie kaisari yaliyo yake na ya Mungu yaliyo yake,”

Amedai kushangaa waraka huo wa salamu za Pasaka kutojikita zaidi katika kuwasisitiza waumini wake kujikita katika kuabudu, kumnyenyekea Mungu, Kusoma biblia na maandiko mengine ya dini na badala yake  wakajikita katika maoni yanayong’ata na kupuliza.

Mwakibinga amesema kwamba kwa sasa nchi imejitanabaisha katika kutatua changamoto zilizokuwa zinasemwa kila siku na wanasiasa hasa wa upinzani ambapo matunda yameanza kuonekana kwa sasa kwani serikali inazishughulikia.

Amewaomba maaskofu kuchagua njia sahihi ya kupita kama walivyofanya wenzao waliowatangulia kwani kuna viongozi wa dini walipoona wanawito wa kushiriki siasa waliamua kuachana na upadri na uaskofu na kujikita kwenye siasa.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search