Mwalimu mbaroni kwa kumkashfu Magufuli...soma habari kamili na matukio360...#shar
Na Mwandishi Wetu, Kagera
MWALIMU wa shule ya sekondari ya Nyakisasa iliyopo mkoani Kagera Deogratias Simon (34) anashikiliwa na jeshi la polisi Kagera kwa tuhuma za kumkashfu rais John Magufuli.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera Augustine Ollom
Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera Augustine Ollom amesema kuwa mwalimu huyo amekuwa akitumia ukurasa wake wa Facebook kuikashfu serikali na rais Magufuli kwa kumuita dikteta na mminyaji wa demkrasia.
"Mwalimu huyu tunashikiliwa kwa kosa la kutumia ukurasa wake wa Facebook kuikashfu serikali na kumkashfu Rais Magufuli kuwa ni Dikteta na anaminya demokrasia," aemsema Kamanda Ollom.
Aidha amesema kwa kuwa yupo mikononi mwao watahakikisha vyombo vya sheria vinatenda haki stahiki dhidi yake ambapo Kamanda amewataka wananchi kuendelea kufichua watu wenye vitendo vya namna hiyo ili wawakabidhi polisi na washughulikiwe
Aidha amesema kwa kuwa yupo mikononi mwao watahakikisha vyombo vya sheria vinatenda haki stahiki dhidi yake ambapo Kamanda amewataka wananchi kuendelea kufichua watu wenye vitendo vya namna hiyo ili wawakabidhi polisi na washughulikiwe
No comments:
Post a Comment