TTCL, Tigo kushirikiana katika huduma za kifedha...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es
Salaam
SHIRIKA la Mawasiliano nchini (TTCL)
limeingia makubaliano ya ushirikiano wa biashara na kampuni ya simu za
mikononi ya Tigo yatakayowezesha wateja wa pande zote mbili kubadilishana fedha
na huduma za kifedha kupitia simu zao za mkononi.
Akizungumza leo
jijini Dar es Salaam kwenye hafla ya kuingia makubaliano hayo, Mkuu wa Huduma za TTCL-Pesa Moses Alphonce amesema kwa kushirikiana na
Tigo katika huduma ya kifedha ya Tigo –Pesa utamwezesha mteja kutuma na kupokea
fedha kwa gharama nafuu.
“Faida za ushirikiano huu,
gharama ni nafuu unapotuma fedha kutoka Tigo-pesa kwenda TTCL-pesa, lakini vile
vile unapotuma fedha kutoka TTCL-pesa kwenda Tigo-pesa,” amesema Alphonce.
Alphonce ameongeza
kwamba kupitia ushirikiano huo utamrahisishia mteja kwani anapotuma au kutumiwa
pesa itaingia moja kwa moja kwenye akaunti yake ambapo amebainisha kuwa lengo
la TTCL-Pesa ni kuhakikisha kila mteja anafikiwa na huduma hiyo.
Amesema kutokana na
huduma hii kufanyika kwa miamala ya simu, wamedhamiria kubadili mifumo ya
malipo yote ya umma na binafsi ili yafanyike kupitia mtandao wa kidigitali na
kuongeza usalama na ufanisi wa shughuli za kiuchumi na kijamii.
Kwa upande wake mkuu
wa huduma za Tigo pesa Hussein Sayed, amesema kuwa Tigo pesa imeazimia kufikisha
huduma sehemu mbalimbali ambazo huduma za kifedha hazijafika ili kuwawezesha
wateja kufanya huduma za kifedha kutoka Tigo-Pesa kwenda TTCL-Pesa kwa kiwango kilekile.
Hata hivyo hatua hii
ya makubaliano kati ya TTCL na Tigo ni muendelezo wa jitihada za shirika la
mawasiliano nchini kurejesha soko la huduma za mawasiliano nchini kwani
hadi sasa TTCL imefanikiwa kufikisha huduma za 4G lite kutoka mikoa 16 ya
Tanzania bara na Visiwa vya Pemba na Unguja.
Mkuu wa Kitengo cha TTCL Pesa
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) Moses Alphonce (kulia) na Afisa Mkuu wa
Kitengo cha Huduma ya Fedha Tigo Hussein Sayed wakipongezana kama ishara ya
uzinduzi rasmi wa huduma za kifedha kwa jia ya mtandao katika ya TTCL Pesa na
Tigo Pesa hafla hiyo imefanyika kwenye Ukumbi Golden Jubilee Tower (PSPF)
jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Kitengo cha TTCL Pesa
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) Moses Alphonce (kulia) na Afisa Mkuu
wa Kitengo cha Huduma ya Fedha Tigo Hussein Sayed wakiwa katika picha ya
pamoja na wafanyakazi wenzao wa TTCL na Tigo mara baada ya uzinduzi huo.
No comments:
Post a Comment