Kandoro afariki dunia...soma habari kamili na maukio360...#share


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MKUU wa mkoa mstaafu Abbas Kandoro amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam alikokuwa amelazwa kwa matibabu.

Kabla ya kifo chake aliwahi kuwa Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Arusha, Singida na Mbeya na mikoa mingine.

Siku mbili zilizopita Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alimtembelea na kumpa pole Mkuu huyo wa Mkoa Mstaafu, Abbas Kandoro ambapo awali alikuwa amelazwa katika hospitali ya Benjamin Mkapa mjini Dodoma kabla ya kuhamishiwa Muhimbili DSM ambapo umauti ndipo ulipomkuta.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search