Mdachi: Vijana changamkieni fursa za mafunzo zinazotolewa na chuo cha NCT...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam


VIJANA nchini wametakiwa kuchangamkia fursa za mafunzo yanayotolewa na Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) ili kuwawezesha  kutapa ujuzi utakaowasaidia kuwapa ajira pamoja na kujiajiri wenyewe.

Mkurugenzi mkuu wa bodi ya utalii Tanzania. Devotha Mdachi akiongea wakati wa ufunguzi  wa tamasha la maonyesho ya la taaluma katika chuo cha taifa cha utalii  (NCT), jijini Dar Es Salaam

Wito huo umetolewa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya chuo hicho Devotha Mdachi alipokuwa akizungumza wakati wa ufunguzi wa tamasha la maonyesho ya  taaluma chuoni hapo.

“Vijana jitokezeni kuchangamkia fursa zinazotolewa na chuo hiki, zitawasaidia  katika kutatua tatizo la ukosefu wa ajira, sambamba na kuwaongeza kipato hivyo kuinua uchumi wa nchi” alisema Mdachi.

Alisema serkali kupitia wizara ya maliasiri na utalii imetoa gari moja dogo ambalo litawasaidia vijana katika kufanikisha utalii wa ndani ikiwa ni sehemu ya  kuunga mkono jitihada za chuo hicho katika kuendelea kutoa mafunzo yanayokidhi viwango vya kitaifa na kimataifa.

Mwenyekiti Wa Bodi Ya Ushauri ya Chuo cha Taifa cha Utalii  Benadeta Nduguru akizungumza wakati wa ufunguzi  wa tamasha la maonyesho ya taaluma katika chuo cha taifa cha utalii  (NCT), April 27 2018 jijini Dar Es Salaam.



Kwa upande wa Mwenyekiti Wa Bodi ya Ushauri ya NCT Benadeta Nduguru, alisema wameandaa tamasha hilo lufatia kutambua umuhimu wa vijana katika kujenga uchumi wa nchi sambamba na kuwakutanisha wadau kutoka taasisi mbali mbali zinazojishughulisha na utoaji wa huduma za kupokea watalii, mahoteli, waongoza watalii hili kuweza kujionea namna chuo hicho kinavyo toa mafunzo yake.

Ndunguru aliongeza kuwa kupitia tamasha hilo wadau wataweza kujionea jinsi chuo hicho kinavyoendesha shughuli zake hivyo kuwa moja ya njia ya kuwawezesha wahitimu wao chuo hicho kupata ajira kwa urahisi.

Tamasha hilo  lilibeba ujumbe usemao "Fursa Za Ajira Kwa Vijana Kupitia Taaluma Ya Ukarimu Na Utalii" ikiwa kama njia ya kuufahamisha uuma juu ya mafunzo yatolewayo katika chuo cha taifa cha utalii.

Mkurugenzi wa chuo cha NCT Sporah  Liana akifafanua jambo katika tamasha la maonyesho ya taaluma katika chuo cha taifa cha utalii  (NCT), jijini Dar Es Salaam.



Wadau kutoka taasisi mbali mbali wakiwasilisha mada katika tamasha la maonyesho ya taaluma katika chuo cha taifa cha utalii  (NCT), April 27 2018 jijini Dar Es Salaam.

Washiriki tamasha hilo kutoka taasisi mbalimbali wakifatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa katika tamasha la maonyesho ya taaluma katika chuo cha taifa cha utalii  (NCT), jijini Dar Es Salaam.

Mgeni rasmi katika tamasha la maonyesho ya taaluma Devotha Mdachi akisikiliza maelezo kutoka kwa wanafunzi wakati alipotembelea mabanda ya wanafunzi hao kujionea namna shughuli zinazofanywa na kuratibiwa na chuo hicho katika tamasha la maonyesho ya taaluma katika chuo cha taifa cha utalii  (NCT), jijini Dar Es Salaam.


Washiriki wa tamasha hilo wakifatilia kwa makini mada ambazo zikiwasilishwa katika tamasha la maonyesho ya taaluma katika chuo cha taifa cha utalii  (NCT), jijini Dar Es Salaam.
Mgeni rasmi katika tamasha la maonyesho ya taaluma Devotha Mdachi akiwa katika picha ya pamoja na vingozi wa chuo icho pamoja na wadau mbalimbali walioshiriki katika tamasha la maonyesho ya taaluma katika chuo cha taifa cha utalii (NCT),  jijini Dar Es Salaam.





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search