Mjema atoboa siri Ilala kufanya vizuri matokeo elimu ya msingi...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

MKUU wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema amesema ukaribu uliokuwepo baina ya walimu na wazazi ndiyo sababu wilaya hiyo kufanya vizuri katika matokeo ya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi 2017.

Mjema amefichua siri hiyo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akitoa tuzo kwa shule za msingi za wilaya hiyo zilizofanya vizuri katika matokeo hayo lengo likiwa ni kutoa motisha kwa walimu pamoja na wadau mbalimbali wa elimu ili kuendelea kufanya vizuri zaidi.

“Halmashauri ya manispaa ya Ilala ilifanya vizuri katika matokeo ya kumaliza elimu ya msingi, ilishika nafasi ya nne kimkoa na nafasi ya pili kiwilaya  hivyo tumeamua kutoa tuzo katika shule hizi ili iwe chachu ya kuongeza Ufaulu,” amesema Mjema. 
 
Amesema tuzo hizo zitawasaidia kuwakumbusha kufanya vizuri ili kufikia nafasi ya kwanza kimkoa na kiwilaya.

Kwa upande wake Ofisa Elimu Msingi Elizabeth Thomas, amesema Idara ya elimu ya Msingi imelenga kutoa tuzo kwa shule zilizofanya vizuri katika matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi (PSLE)  mwaka 2017 zenye lengo la kutoa motisha nakuwapongeza walimu kwa kazi kubwa ya ufundishaji na ujifinzaji waliofanya na kuzaa matunda ya matokeo mazuri.

Amesema Jumla ya shule 184, zikiwemo za Serikali 107 na zisizo za Serikali 77,ambapo jumla ya wanafunzi 21,704 walisajiliwa kufanya mtihani wakiwemo wavulana 10,270 na wasichana 11,434.

Aidha wanafunzi waliofanya mtihani walikuwa 21,569 wavulana 10,184 na wasichana 11,365 sawa na asilimia 99.3% waliofaulu ni wanafunzi 19,236 wakiwemo wavulana 9,199 na wasichana 10,037 sawa na asilimia 89% na wanafunzi wote hao wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka 2018.

Amebainisha kuwa tuzo hizo zimetolewa katika makundi mbalimbali zikiwemo shule  kumi bora,shule zilizopandisha ufaulu zaidi ukulinganishwa na ufaulu wa mwaka 2016, kata iliyofanya vizuri, shule zilizofanya mtihani  kwa Mara ya kwanza na zikafanya vizuri pamoja na kutoa tuzo maalumu kwa wadau mbalimbali.

 




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search