Mwili wa Mama Gambo kuzikwa Uru...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Arusha

Mama wa Mkuu wa mkoa Arusha, Mrisho Gambo anatarajiwa kuzikwa Uru mkoani Kilimanjaro baada ya mwili wake kurejeshwa nchini.

Katibu Tawala Mkoa Arusha, Richard Kwitega alisema hayo wakati akizungumza katika dua maalum leo, Aprili 14, iliyofanyika nyumbani kwa Mkuu wa Mkoa.

Kwitega amesema "mwili wa  marehemu Rehema Momburi, unatarajiwa kuwasili Jumanne kutoka nchini India,".

Kwa mujibu wa ratiba, mazishi yatafanyika Alhamisi  ya wiki ijayo.

Viongozi mbalimbali wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa, umoja wafanyabiashara, wakurugenzi, mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema na viongozi wengine kadhaa walihudhuria.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search