Profesa Mkumbo akosoa waraka wa Maaskofu KKKT...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Maji, Profesa Kitila Mkumbo
amemwandikia barua Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Askofu
Frederick Shoo kuhusu maudhui ya waraka wa maaskofu wa kanisa hilo uliotolewa hivi karibuni.
Profesa Kitila Mkumbo
Katika waraka huo Profesa Mkumbo amsema ni maoni yake binafsi kwa kanisa hilo.
Waraka wa maaskofu 27 wa KKKT ulitoka hivi karibuni na
ulitarajiwa kusomwa katika makanisa yote ya kilutheri Machi 25, 2018.
Katika waraka huo maaskofu walizungumzia Katiba mpya,
uchumi, siasa na jamii.
“Katika kutoa maoni yangu kuhusu Waraka huo, ninalenga mambo
makubwa mawili ambayo ni pongezi kwenu, na pili ni mtazamo wangu juu ya baadhi
ya masuala yaliyomo katika Waraka huo,” amesema Kitila katika barua yake
aliyoisaini Machi 29 mwaka huu.
Pamoja na kuwapongeza maaskofu hao, Kitila ameandika katika
barua yake kuwa maudhui yaliyowekwa katika waraka wa maaskofu hao, hayaakisi
hadhi na wajibu wa msingi wa kanisa.
“Kama ambavyo mmekuwa mkitufundisha siku zote, na vile tusomavyo
katika Biblia Takatifu, ninafahamu kuwa kazi za msingi za kanisa ni zile ambazo
Bwana wetu Yesu Kristo alizifanya alipokuwa duniani,”amesema.
Kitila ambaye ameandika barua hiyo kama muumini wa KKKT, amesema
anakubaliana na mengi maaskofu waliyogusia katika Waraka huo akiamini yamefundisha
na kuponya roho za waumini kwa kiasi kikubwa.
Hata hivyo, alichambua hoja katika maeneo matano zilizoibuliwa
na maaskofu hao na kusema ni sahihi lakini akatahadharisha kuwa ni muhimu kwa
kanisa kujiepusha na kuonekana lipo upande fulani katika mijadala ya kitaifa
inayogusia jamii.
“Kwa kufanya hivyo, mtaepusha migawanyiko isiyo ya lazima kwa
waumini ndani ya kanisa na wananchi kwa ujumla.” Amesema.
Amesisitiza kuwa ni muhimu kwa kanisa kupima kwa umakini mkubwa
uzito wa kila neno kabla ya kutoa kauli katika umma.
“Ni hatari kwa Kanisa kutoa kauli inayosababisha maumivu na
mifarakano badala ya kuponya.”
No comments:
Post a Comment