Sakata la Nondo kutekwa latua Bungeni...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MBUNGE wa CUF, Dk. Suleiman Ally Yussuf  amehoji ni sababu zipi zilizofanya  Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo kuwekwa mahabusu ya Polisi kwa kipindi kirefu bila ya kufikishwa Mahakamani kusomewa mashtka

Dk. Suleimani amehoji hayo leo  katika Mkutano wa 11 wa kikao cha Bunge cha kwanza kinachoendelea kufanyika katika mkoa wa Dodoma wakati alipokuwa anauliza swali ya nyongeza kwenda kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ambapo alitaka kufahamu uhalali wa Jeshi la Polisi juu ya kuwashikilia watuhumiwa.

"Wako watu wengi wanaowekwa mahabusu ya Polisi kwa zaidi ya siku 15 bila ya kupelekwa Mahakamani akiwemo mwanafunzi Abdul Nondo. Nataka nijue ni sheria gani ambayo inatumika au inatumiwa na Jeshi la Polisi kuwaweka watu mahabusu ya Polisi zaidi ya muda huo mrefu bila ya kupelekwa Mahakamani", amehoji Dkt. Suleiman.

Aidha, katika kujibu hoja hiyo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amesema polisi ni chombo kilichoundwa kwa mujibu wa katiba na sheria na linatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba.

"Polisi wana mamlaka kisheria kutuhumu, kukamata, kuhoji na kuweka watuhumia mahabusu kwa muda ulioruhusiwa kisheria endapo itabainika kuwa kuna viashiria au taarifa ya kuhusika katika kutenda kosa la jinai. 

"Kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za utendaji zinazoongoza Jeshi la polisi inapobainika askari amembambika kesi kwa sababu zozote zile huchukuliwa hatua mbalimbali za kinidhamu ikiwemeo kufukuzwa",amesema Waziri Mwigulu.

Pamoja na hayo, Waziri Mwigulu ameendelea kwa kusema "kwa kuwa jambo la kiusalama ni kipaumbele, kwa mtuhumiwa na rai wengine waliosalia, Jeshi la Polisi hutumia wajibu wake waliopewa wa kulinda usalama wa raia kwa kuweza kuhakikisha kwamba linatimiza majukumu yake na huku likiwaacha watu wakiwa salama kabisa".

Kwa upande mwingine, Waziri Mwigulu hakuweza kujibu suala lolote kuhusu Nondo kama jinsi lilivyo hojiwa na Mbunge Sulleiman juu ya uhalali wa Jeshi la Polisi kumuweka kijana huyo zaidi ya siku 15 mahabusu ya polisi.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search