Chuo cha NIT chapandishwa hadhi ya chuo kikuu...soma habari kamili na matukio360...#share

Na
Abraham Ntambara
SERIKALI
imekipandisha hadhi Chuo cha
Usafirishaji nchini (NIT) kuwa chuo kikuu ambapo hivi karibuni kinatarajia
kuanza kutoa elimu ya shahada ya kwanza.
Pichani Kushoto ni Mkuu wa Chuo
cha Usafirishaji nchini (NIT),Profesa Zacharia Mganilwa,akikabidhiana
makubaliano ya ushirikino baina ya Chuo hicho na Chuo cha Usafirishaji nchini
Korea ,na Profesa Woo Jongwouk , ambaye alimwakilisha Profesa Lee Byungchan
naye ni Rais wa Chuo kikuu cha Usafirishaji nchini Korea,makubaliano hayo
yamefanyika leo Jijini Dar es Salaam.
|
Hayo
yamebainishwa leo Jijini Dar es Salaam na Mkuu wa chuo hicho, Profesa
Zacharia Mganilwa, wakati wa halfa fupi ya kutiliana saini ya Ushirikiano baini
ya Chuo cha NIT na Chuo cha Usafirishaji nchini Korea.
“Katika
kuimarisha sekta ya usafirishaji nchini, serikali ilikipandisha hadhi chuo hiki
ya kuwa chuo kikuu, na kitaanza kutoa elimu ngazi ya shahada,” amesema Profesa
Mganilwa.
Akizungumzia
kuhusu makubaliano walioingia baina ya vyuo hivyo, amesema makubaliano hayo ni
kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa Walimu wa
chuo cha NIT ili waweze kupata ujuzi wa jinsi ya kusimamia Usafiri wa Treni
ambazo zinatumia Umeme.
Profesa Mganilwa ameongeza kwamba katika makubaliano hayo yatakisaidia chuo hicho kutoa Walimu wenye shahada ya kwanza kwenda nchini Korea kusomea Shahada ya uzamili ya masuala ya usafirishaji wa Treni za kisasa.
"Katika
makubaliano haya Walimu wenye Shahada ya kwanza watapata fursa ya kwenda nchini
Korea kwenda kupata Ujuzi wa Masuala ya Usafirishaji wa Uendeshaji Treni za
Umeme ili waje kutoa elimu kwa Vijana wetu hapa nchini"Amesema Profesa
Mganilwa .
Profesa
Mganilwa amesema Mafunzo hayo kwa Walimu hao yanataisadia nchini kwa sasa
ambapo inaingia katika usafiri wa Treni za kutumia mfumo wa Umeme ambapo
mradi wake unaanza kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro.
Amesema
kwa sasa katika chuo hicho wana Walimu wachache wenye ujuzi wa kufundisha
Wanafunzi katika uendeshaji wa Treni za Umeme.
"Hapa
Chuoni tuna Walimu wachache wa hivyo kuongezeka kwa walimu hama kutasaidi
kupanuka kwa ufundishaji Wanafunzi hawa ambapo wataweza kusimamia
hizi"Ameongeza kusema.
Hata
Hivyo ,Profesa Mganilwa amesema makubalino hayo yanakuja ikiwa ni teyari
Serikali imeshakipandisha Hadhi chuo hicho na kuwa cha Usafirishaji huku
akiwaka wanafunzo wote wanaohitimu kidato cha nne na Cha Sita kuhakikisha
wanajitokeza katika kusomea masomo ya usafirishaji wa njia ya Reli.
Kwa
Upande wake, Profesa Woo Jongwouk , ambaye alimwakilisha Profesa Lee Byungchan
naye ni Rais wa Chuo kikuu cha Usafirishaji nchini Korea,amesema wataendelea
kushirikiana na Chuo cha NIT katika kutoa watalaamu mbali mbali katika usafirishaji.
"Tunafarijika
na ushirikiano huu mzuri,na tunawahaidi tutaendelea kushirikiana na Chuo hichi
katika kuzalisha wataalamu "Amesema Profesa Jongwouk.
No comments:
Post a Comment