Majaliwa aagiza wizara, mashirika na taasisi kutumia nishati mbadala...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara,  Dar es Salaam

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ameziagiza wizara, mashirika na taasisi zote za Serikali na binafsi zianze kutumia nishati mbadala ili kuondoa kabisa matumizi ya kuni na mkaa.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipozindua Wiki ya Mazingira  kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.

Ametoa agizo hilo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua wiki ya mazingira duniani ambayo kitaifa imefanyika jijini hapa, ambapo amesisitiza juu ya utunzaji wa mazingira

“Nitoe maagizo kwa wizara, ashirika na taasisi zote za serikali na binafsi zianze kutumia nishati mbadala ili kuondoa kabisa matumizi ya kuni na mkaa,” amesema Waziri Mkuu Majaliwa.

Aidha amewataka wananchi kutunza na kuhifadhi mazingira yao na kujiepusha na tabia ya kukata miti hovyo, ikiwemo kutupa taka ngumu hovyo katika maeneo yanayowazunguka. 

Waziri Mkuu Majaliwa amesema kuwa  ni wajibu wa kila mwananchi kutunza mazingira na kuwataka watanzania kutimiza wajibu huo.

“Kwa nzia sasa kila mtanzania anatakiwa  kutumia mkaa mbadala, ili kuhifadhi misitu na kupunguza uharibifu wa mazingira,” amesema.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano January Makamba amesema lengo la kuadhimisha siku hii ni kuhamasisha na kuelemisha wananchi kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira.

“Lengo la kuadhimisha siku hii ni kuhamasishana na kuelimishana kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira, mwaka huu maadhimisho haya yanachukuliwa kwa umuhimu mkubwa kutokana uharibifu mkubwa wa mazingira,” amesema Makamba.

Amesema pia lengo la kufanyia maadhimisho hayo jijini Dar es Salaam kwa mwaka huu ni kutokana na jiji hilo kuwa  kitivo cha uchumi wa nchi ambapo asilimia 70 ya mkaa wa kuni unatumika.

Waziri Makamba amesema Serikali ina mpango wa kupunguza matumizi ya kuni na mkaa kutoka asilimia 50 hadi 36, na kwamba hiyo ndio faida ya kutumia majiko ya vumbi la makaa ya mawe kwa kuhifadhi mazingira.

Nao baadhi ya  wadau wa mazingira wameahidi  kuendelea kushirikiana na Serikali katika mapambano ya kulinda na kuhifadhi mazingira

Siku ya mazingira duniani kitaifa imeambatana na maonyesho mbalimbali ya  teknolojia ya uzalishaji wa mkaa mbadala.

Matukio mbali mbali katika picha.









About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search