HATIMAYA JAY DEE AWEKA WAZI 'STATUS' YAKE !!

Lady Jay D na Spicy.
WAKATI akitarajia kuzindua albamu yake ya saba Ijumaa hii, mkongwe wa Afro Pop Bongo, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ amewataka wabongo kuacha kuwaziana mabaya, kwani wengi wao wanapenda wenzao waharibikiwe.



Lady Jay D.
Alitoa kauli hiyo baada ya kuulizwa ukweli kuhusu kuachana kwake na mpenzi wake raia wa Nigeria, Spicy, kufuatia maandishi

aliyoandika katika akaunti ya mtandao wake wa Instagram, wiki tatu zilizopita, ulioashiria kuwepo kwa matatizo kwenye uhusiano wake.

“Niko vizuri na Spicy, yale maneno niliandika kwa ajili ya muziki, watu wanapenda kuona wenzao wanaharibikiwa, kwa nini wanakimbilia kuamini nina matatizo na Spicy na hawafikirii kuhusu kazi yangu? Niwakaribishe waje kwenye shoo yangu ya uzinduzi pale Lugalo Uwanja wa Gofu Ijumaa hii,” alisema Jide.

Collected from: http://www.williammalecela.com


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search