DR CONGO WAPATA WAZIRI MKUU MPYA; NI BRUNO TSHABALA

Bruno Tshibala ndiye waziri mkuu mpya DR Congo

Bruno Tshibala - waziri mkuu mpya DR Congo

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Joseph Kabila, amemteua Bruno Tshibala kama Waziri Mkuu mpya katika Serikali ya kugawana madaraka.
Bwana Tshibala ataongoza taifa hilo hadi uchaguzi wa Urais unaotazamiwa kufanywa baadaye mwakani.
Alitimuliwa kutoka chama kikuu cha upinzani, UDPS, mwezi uliopita baada ya kupinga watu waliochaguliwa chamani kuchukua madaraka ya kiongozi aliyefariki Februari, Etienne Tshisekedi.
Waandishi wa habari wanasema kuwa kuchaguliwa kwa Bwana Tshibala kutawagawanya zaidi wapinzani wa Bwana Kabila baada ya mashauriano ya kujadili jinsi atakavyoondoka mamlakani kuporomoka juma lililopita.

Souce: bless news

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search