Lil Wayne afunguka kuhusu mpango wa kujiunga na lebo ya Jay Z


Lil Wayne ameweka wazi kinachoendelea kati yake na Jay Z, ikiwa ni siku chache baada ya kusikika kwenye tamasha akisema ‘It’s the Roc’, sentensi ambayo ilitafsiriwa na wengi kuwa alimaanisha anajiunga na ‘Roc Nation’ ya nguli huyo.
Kauli hiyo ya Lil Wayne iliibua mengi kutokana na ukweli kuwa ana mgogoro mzito kati yake na bosi wake Birdman na amewahi kutaka kuachana naye akimtuhumu kumkandamiza kifedha na kumrudisha nyuma.
Akifunguka hivi karibuni kwenye kipindi cha Undisputed cha FS1, Lil Wayne alisema kuwa Jay Z ni mtu mwema sana na kwamba amekubaliana naye kuwa atamsaidia tu.
“Jay ni mtu mwema. Hakukuwa na kitu lakini ni rahisi tu kati ya rafiki na rafiki yake, ‘ninataka kukusaidia tu’,” alisema akimkariri Jay Z. “Kirahisi tu, na ndivyo ilivyokuwa, ‘ninataka nikusaidie kadiri niwezavyo’. Hivi sasa atanisaidia, hivyo ndivyo ilivyo,” aliongeza.
Hata hivyo, alikanusha kuwa anapanga kuhamia kwenye ngome ya Roc Nation kama inavyoelezwa na wengi. Alisisitiza kuwa bado wanaendelea kutafuta ufumbuzi wa tatizo lao yeye na bosi wake Birdman akiwa chini ya Cash Money.
Source habari 5

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search