MAPOROMOKO YALETA MAAFA COLOMBIA; 250 WAKADIRIWA KUPOTEZA MAISHA

Mamlaka ya jeshi la Colombia inasema idadi ya waliofariki katika maporomoko ya ardhi nchini humo imefikia watu 250 huku waliojeruhiwa wakiwa 400.
Hata hivyo idadi hiyo huenda ikaongezeka kwani bado kuna zaidi ya watu 200 ambao hawajapatikana . 
Vikosi vya wafanyikazi wanaoendesha shughuli za uokoaji wanasema nyingi ya barabara za kulipotekea maporomoko hayo huko eneo la mji wa kusini mwa taifa hilo, Mocoa hazipitiki kutokana na mkasa huo. 
Watu 250 waangamia kwenye maporomoko ya ardhi ColombiaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionWatu 250 waangamia kwenye maporomoko ya ardhi Colombia
Maporomo hayo yametokea baada ya mvua kali kunyesha kwa saa nyingi. 
Viongozi wa mataifa jirani wa Mexico na Argentina walikuwa wa kwanza kutoa ujumbe wa pole na kuahidi kwenda kuisaidia Colombia.
Rais Juan Manuel Santosa alitangaza hali ya tahadhari eneo hilo na kusafiri kuangalia shughuli za uokoaji.
Watu 250 waangamia kwenye maporomoko ya ardhi ColombiaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionWatu 250 waangamia kwenye maporomoko ya ardhi Colombia
Picha zilizochapisww kwenye mitandao na jeshi zilionyesha baadhi ya majeruhi wakiokolewa kwa kutumia ndege.
Maporomo koya ardhi yamekumba eneo hilo mara kadha miezi ya hivi karibuni.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search