Video: Ona Nape 'alivyojidai-dai' Bungeni, asema "tuna hatari ya kutorudi Bungeni uchaguzi ujao.."

Katika hali iliyoonekana kujifaragua katika nafasi yake ya Ubunge, Mbunge wa Mtama Mhe. Nape Nnauye amekosoa vikali kipaumbele cha serikali katika kuhakikisha maji yana wafikia Wananchi Vijijini hasa wanawake ambao ndio wapiga kura wengi walioiweka serikali ya CCM madarakani.

Mbunge wa Mtama ambaye pia alishawahi kuwa Waziri wa Habari, utamaduni, Sanaa na Michezo hakuonyesha woga kuikosoa bajeti ya Wizara husika jambo ambalo ni tofauti na wakati alivyokuwa na kofia ya Uwaziri ambapo alikaa benchi moja na Waziri muhusika.
 Nape Nnauye ameliambia Bunge kuwa katika ilani ya CCM wakati wa uchaguzi waliwaahidi wananchi kuwa watatatua changamoto za maji lakini hadi sasa bado hatua stahiki hazijachukuliwa. hivyo endapo tatizo halitoangaliwa na kutatuliwa CCM ijue wananchi hawatairudisha tena madarakani. 
Full video ya mchango wa Endelea kumsikiliza nape katika video hapa chini...



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search