Habari mpya za hivi punde: Wahalifu wamewajeruhi watu wawili kwa Risasi na kisha kuondoka na majeruhi hao..
Taarifa mpya zilizotufikia hivi punde kutoka mkoa wa Pwani zinasema, taarifa kutoka Jeshi la pilisi mkoa huo ni kwamba wahalifu wamewapiga risasi watu wawili kisha kuondoka na majeruhi hao... amethibitisha Kamanda wa Polisi Mkoa RPC Onesmo Lyanga.
Tunaendelea kufuatilia taarifa hizi usikae mbali kupitia.. www.matukiotza.blogspot.com
=========================================================
Mapema leo asubuhi Blog yako ya Matukio iliripoti uwepo wa vifo vya watu watatu kwenye tukio hilo.
__________________________________________________________
Kuna Taarifa ya kusikitisha tumeipokea hivi punde ambapo watu watatu wakazi wa Kijiji cha Nyamisati katika kata ya Salale wilayani Kibiti wanasadikiwa kufariki dunia kwa kupigwa risasi usiku wa kuamkia Leo.
Mkazi mmoja wa Kijiji hicho aliyejitambulisha kwa jina moja la Hamza amesema miongoni mwa watu waliopigwa yumo mwanamke mmoja ambaye ni mwenyekiti wa kitongoji kimojawapo kijijini hapo.
Watu hao wanaosadikiwa kupoteza maisha ni Hamid Kidevu,Yahaya Mkame na Moshi Machela.
Mkuu wa wilaya ya Kibiti Gullamuhusein Kifu amesema ameliagiza jeshi la Polisi wilaya hapa kwenda eneo hilo kwa ajili ya uthibitisho.
Matukio blog tunaendelea kukupasha yatakayojiri baada ya taarifa ya Jeshi la Polisi.
Source- Mcl digital
Tunaendelea kufuatilia taarifa hizi usikae mbali kupitia.. www.matukiotza.blogspot.com
=========================================================
Mapema leo asubuhi Blog yako ya Matukio iliripoti uwepo wa vifo vya watu watatu kwenye tukio hilo.
__________________________________________________________
Mkazi mmoja wa Kijiji hicho aliyejitambulisha kwa jina moja la Hamza amesema miongoni mwa watu waliopigwa yumo mwanamke mmoja ambaye ni mwenyekiti wa kitongoji kimojawapo kijijini hapo.
Watu hao wanaosadikiwa kupoteza maisha ni Hamid Kidevu,Yahaya Mkame na Moshi Machela.
Mkuu wa wilaya ya Kibiti Gullamuhusein Kifu amesema ameliagiza jeshi la Polisi wilaya hapa kwenda eneo hilo kwa ajili ya uthibitisho.
Matukio blog tunaendelea kukupasha yatakayojiri baada ya taarifa ya Jeshi la Polisi.
Source- Mcl digital
No comments:
Post a Comment