Makamu Samia alivyobariki 'arobaini' cha Makokoro Mwanza !

Maelfu  ya nyavu aina ya kokoro zinazotumika kutekeleza uvuvi haramu Jijini Mwanza na vitongoji vyake leo yalitimiza 'arobaini' yake baada ya Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan kuongoza zoezi la kuteketeza jumla ya nyavu 5662 za uvuvi haramu katika Dampo la Buhongwa. 

Akiongea mara baada ya kukamilisha awamu ya kwanza ya zoezi hilo, Mama Samia amewataka viongozi wa Mkoa huo na Mikoa jirani kushirikiana na kuwachukulia hatua kali wanaojihusisha na vitendo hivyo.

Amesema amesema Mungu amewawekea ziwa wakazi wa maeneo hayo kwa makusudio yake, na Serikali haitavumilia kwa namna yoyote ile uharibifu wa rasilimali za ziwa hilo na kuwataka kulitunza. 

Nae Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella amesema wameanza kuchukua hatua kwa baadhi ya watendaji wanaobainika kuhusika na vitendo hivyo.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search