Neno la Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Mutungi Baada ya Taarifa za Maalim kuhamia Ofisi Mpya za kisasa - Magomeni !!

“Naamini Chama cha CUF kitafanya mambo yake kwa mujibu wa kuzingatia sharia zinazoongoza mwenendo wa Vyama vya Siasa Nchini…” 

Taswira ya Jengo jipya na la kisasa zilipo Ofisi kuu za Chama cha CUF
Hayo ni maneno ya Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi akitoa ‘neno’ baada ya kuzagaa kwa taarifa za Maalim Seif kufungua na kuendesha ofisi za chama hicho maeneo ya Mtaa wa Idrissa mjini Magomeni Mapipa – Jijini Dar es Salaam.
Hata hivyo, Jaji Mutungi amesema hajapata taarifa yoyote rasmi ya chama hicho juu ya kufungua ofisi mpya mbali na kuyasikia kupikia vyombo vya habari.

"Ukiondoa taarifa za kwenye media sijapata taarifa yoyote kutoka CUF labda wawe wameleta leo (jana), lakini naamini chochote wanachofanya wanaelewa taratibu wataleta taarifa,”amesema Jaji Mutungi.... Msajili amesema sheria inawataka wanapofungua ofisi watoe taarifa ndani ya siku 14, ambazo hazijaisha hivyo anaamini wanajua hilo.

Kwa mujibu wa taarifa zinazoendelea kusikika, Upande wa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad uamefungua ofisi hizo, baada ya tukio la kuvamiwa katika Ofisi Kuu za Buguruni na kundi linalotambulika na ofisi ya Msajili la Profesa Ibrahim Lipumba.


Jaji Mutungi amesema atakapopokea taarifa rasmi ataangalia kama taratibu zikifuatwa kwani ufunguaji wa ofisi mpya una taratibu zake. “Nikiletewa taarifa ndio nitajua kama walifata taratibu au la, ufunguaji wa ofisi una taratibu zake najua wanazijua pia,” alimalizia Jaji Mutungi.- masaa 24

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search