Nyama ya 'Kitimoto' yaleta shida huko Dodoma.. #SHARE Manispaa wasema kuna 'mlipuko' !!

Manispaa ya Dodoma ambapo ndipo yalipo Makao Makuu ya Nchi, imetoa tahadhari kwa walaji na wauzaji wa nyama ya Nguruwe,  almaarufu kama kitimoto.


aina ya kitimoto wanaopatikana nchi za baridi !
Akitangaza tahadhari maalum kupitia taarifa rasmi aliyoisaini yeye mwenyewe, Afisa Habari wa Manispaa hiyo Bw. Ramadhani Juma, amesema kwa sasa kumebainika uwepo wa ugonjwa unaotambulika kitaalamu kama 'Homa ya Nguruwe', hivyo shuguli yoyote inayohusu biashara ya kitimoto na jamii zake lazima ifanywe kwa kibali maalum cha Manispaa.

Afisa Habari huyo alimalizia kwa kuwataja wanyama wengine wanaohusika na 'marukuku' hiyo kuwa ni pamoja na ngiri na nguruwe pori.


Matukio blog imefanikiwa kunasa taarifa rasmi ya Manispaa na kukuletea kwenye ukurasa huu.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search